Yvette Obura alikuwa mpenzi wa staa huyu na wakapata mtoto (Mueni)
Haya yamejiri baada ya msanii huyu kumtaka mzazi mwenzake Yvette kuweka wazi ni kwani nini alitumia treni ya SGR kuenda mjini Mombasa.
Yvette alimjia juu na kusema kuwa iwapo anahisi kuwa kupanda treni kunashusha hadhi yake, basi amnunulie mtoto wake Mueni ndege ya kusafiria.
"Kwa hivyo Bahati anadhani kuwa binti wake hawezi kupanda treni? Kwa sababu ana hela nyingi basi amnunulie ndege...' Alisema Obura.
Bahati amezaa mtoto Mueni Bahati na Obura,
Katika mahojiano ya jadi, Obura alisimulia jinsi kulea mtoto huyu na Bahati kunakuwa changamoto.
“Co-parenting si rahisi, you know he has wife halafu maybe am in another relationship, alafu unajua kuna zile time hatuwezi pigiana simu ati Mueni anataka hii. Sisi wote ni vichwa ngumu..." Alisimulia Obura.