'Nina mpenzi ambaye nampenda sana,' Hamisa Mobetto asema
- Fred Vunjabei ni zaidi ya ndugu yangu nina mpenzi ambaye nampenda sana hamisa azungumzia uhusiano wake na Fred
Hamisa Mobetto ameweka mamboo wazi kuwa ana mpenzi na wala si Fred Vunjabei, hii ni baada ya uvumi kuenea kuwa wawili hao wamo katika uhusiano wa kimapenzi.
Akiwa kwenye mahojiano, Hamisa alisema kuwa anampenzi ambaye ana mpenda sana na Fred ni ndugu yake wala si mpenzi wake.
"I have a boyfriend. Nina mpenzi ambaye Nampenda sana na sio Vunjabei. Sio mpenzi wangu. Yeye ni bro, yaani mshikaji wangu nikiwa na idea fulani ya biashara ama yeye akiwa anataka staff fulani katika biashara yake ananitafuta. Other than that hakuna uhusiano ni mtu mpoa sana." Hamisa Alisema.
Wiki jana mwanamitindo Hamisa alifichua jinsi alivyo beba mimba tatu za msanii Diamond huku zikitoka moja baada ya nyingine.
Kwa upande wake Vunjabei alikuwa na haya ya kuzungumzia kuhusu uhusiano wake na Hamisa.
"Watu wanafikiria ni mpenzi wangu. Sio mpenzi wangu. Mimi na yeye hatuna mahusiano. Ni mshikaji wangu mno. Mpaka juzi kati nilikuwa na muuliza mbona ako single, akaniambia anaenjoy Sana kuwa single kuliko kuwa na mahusiano. Anasema akiwa na mahusiano anahisi kama una utetemesha moyo wake. Ame amua kulerax afanye kazi kwanza." Alieleza Vunjabei.
The video could not be loaded.