logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Naamini atamuonyesha kaburi la baba yake,'Mzee Abdul amwambia Mama Dangote

Mzee Abdul alikumbuka jinsi alimsaidia Mama Dangote wakati Diamond alipokuwa mchanga

image
na Radio Jambo

Yanayojiri18 January 2021 - 10:12

Muhtasari


  • Mzee Abdul asema kwamba mama Dangote hakumwambia kwamba ujauzito si wake
  • Pia alisema kwamba anaamini mama huyo atamuonyesha msanii huyo kaburi la baba yake
  • Abdul alifichua kwamba alimsaidia mama Dangote enzi hizo alipokuwa tajiri
Mzee-Abdul

Familia yake staa wa bongo Diamond Platnumz imekuwa kwenye vichwa vya habari punde tu mama yake alipofichua kwamba mzee Abdul si baba yake diamond.

Mama yake Diamond, alipost picha Instagram za mwanamume kwa jina Salim Idi Ny'ange, anayedai ni baba halali wa mmiliki huyo wa Wasafi Records.

Mzee Abdul ameweka wazi kwamba anatumai kwamba mama Dangote atamuonyesha msanii huyo kaburi la baba yake.

 

"Naachia yote mwenyezi Mungu, naamini kwamba mama yake ataenda kumuonyesha kaburi la baba yake, nafikiri wangeniita katika mkutano wa kifamilia ili kufichua habari hizi badala ya kuzifichua kwa umma." Abdul Alizungumza.

Mzee Abdul alikumbuka jinsi alimsaidia Mama Dangote wakati Diamond alipokuwa mchanga kwa maana hakuwa na mtu yeyote wa kumsaidia.

"Ukweli nilikuwa tajiri, nilimsaidia kifedha alikataa kunambia kwamba ujauzito si wangu kwa maana hakuwa na pesa

Alifikiria kuwa hamna mtu ambaye atamsaidia akisema ukweli ."

Mzee Abdul na Mama Dangote waliachana msanii huyo akiwa kidato cha kwanza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved