In Summary
  • Msanii Loise Kim alaumu vipasa sauti kwa kusambaza virusi vya corona miongoni mwa wahubiri na wasanii
  • Usemi wake ulijiri saa chache baada ya mwandishi wa habari katika kampuni ya Royal Media Robin kuaga dunia kutokana na virusi hivyo
Loise KIm
Image: Instagram

Msanii wa nyimbo za kikuyu Loise Kim kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram alilaumu vipasa sauti kwa kusambaza virusi vya corona miongo mwa wahubiri, wasanii na hata wanahabari.

Usemi wake ulijiri saa chache baada ya mwandishi wa habari katika kampuni ya Royal Media Robin kuaga dunia kutokana na virusi hivyo.

Pia usemi wake ulijiri baada ya muhubiri maarufu na msanii wa nyimbo za kikuyu Mercy waciama kuaga dunia iliyodaiwa aliaga dunia  kutokana na virusi hivyo.

 

Ni mwaka mmoja tangu kisa cha kwanza cha virusi vya covid-19 kutangazwa nchini, huku zaidi ya watu elfu moja wakiangamizwa na virusi hivyo.

Kulingana na msanii huyo wasanii wengi wanaoaga dunia kutokana na virusi hivyo ni kwa ajili ya vipasa sauti ambavyo wanatumia wakiburudisha mashabiki wao.

"Wahubiri na waimbaji wengi wameshindwa na mnyama huyu,Nadhani vipasa sauti ni bingwa katika usambazaji wa corona Ikiwa haijasafishwa vizuri tunaweza kuishia kuwapoteza wengi Kwaya za kanisa, wakuu wa sherehe, wanahabari na kadhalika  jilindeni ni utafiti wangu," Alisema.

Je maoni yako kuhusu usemi wake Loise ni yapi, na je unafikiri kwamba vipasa sauti zinasambaza virusi hivyo kwa kasi sana na kwa idadi kubwa?
View Comments