logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Hamna haja kutoa taarifa kuhusu yaliyo wazi' Juliani avunja kimya kuhusu madai kuwa anachumbia aliyekuwa mke wa gavana Mutua

Picha kadhaa  za msanii huyo akijivinjari na Lilian zimekuwa zikienezwa mitandaoni na kusemekana kuwa wamejitosa kwenye uhusiano wa kimapenzi.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri01 September 2021 - 07:26

Muhtasari


•Picha kadhaa  za msanii huyo akijivinjari na Lilian zimekuwa zikienezwa mitandaoni na kusemekana kuwa wamejitosa kwenye uhusiano wa kimapenzi.

Mwanamuziki Julius Owino almaarufu kama Juliani hatimaye amejitokeza kuzungumzia madai kuwa anachumbia aliyekuwa mke wa gavana Alfred Mutua Bi Lilian Ng'ang'a.

Tangu Mutua na Lilian watangaze kuvunjika kwa ndoa yao mwezi uliopita uvumi  umekuwa ukitanda mitandaoni kuwa msanii huyo ndiye sababu kuu ya kutengana kwao.

Picha kadhaa  za msanii huyo akijivinjari na Lilian zimekuwa zikienezwa mitandaoni na kusemekana kuwa wamejitosa kwenye uhusiano wa kimapenzi.

Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, msanii huyo amechapisha ujumbe wa kimafumbo na kusema kuwa watu wana uhuru wa kufikiria wanavyotaka.

Baba huyo wa mtoto mmoja aliyepata na aliyekuwa mpenzi wake mwigizaji Brenda Wairimu amesema kuwa hakuna haja yake kutoa taarifa kuhusu jambo ambalo ni wazi.

"Asante sana kwa wale ambao wamewasiliana nami ndani ya kipindi cha wiki chache zilizopita. Mola awazidishie.

Hakuna haja ya kutoa taarifa kuhusu suala ambalo ni wazi. Najua mnaweza jiwazia wenyewe. Pateni hitimisho wenyewe. Nawaaminia" Juliani ameandika kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved