Nimechoka kuandikwa mabaya-Amber Ray aghadhabishwa na video yake iliyopakiwa mitandaoni
- Amber Ray agadhabishwa na video yake iliyopakiwa mitandaoni
Mwanasosholaiti Amber Ray ametoa elfu mia tatu kwa mtu ambaye atafichua shabiki ambaye alipakia video yake alipokuwa kwenye hoteli ya Miale.
Mamahuyo wa mtoto mmoja alishirikisha chapisho kwenye ukurasa wake wa Instagram akisema kuwa yuko tayari kutoa fedha kwa kiasi cha mia tatu elfu kwa mtu yeyote ambaye atafichua shabiki ambayealirekodi video alipokuwa na meneja wake.
Amber Ray alishiriki video ya sekunde 30 kwenye ukurasa wake na kusema kwamba yeye hajafurahi baada ya kujifunza kwamba mmoja wa mashabiki wake alichukua video yake wakati akiwa na wakati wa kibinafsi na mameneja wake.
Mwanasoshalaiti huyo alidai alikuwa na mameneja wawili wa kiume na wa kike na shabiki tu alizingatia meneja wa kiume tu kumfanya aonekane mbaya.
Pia amesema kwama amechoka na wanamitandao kuchapisha hadithi mbaya kumhusu kila wakati.
"Nimeona video hii kwenye moja ya makundi ya uvumi ... lakini wakati huu karibu, nimechoka na wewe kuchapisha upuzi kwa ajili yangu ... Yaaani nina mameneja wangu 2 juu ya kuweka (kiume na kike) lakini unachagua kuandika yasiyo na maana juu yangu ili nionekane mbaya kama kawaida ... kama unavyojaribu kula, tunapaswa kuheshimiana
Kama unamjua aliyerekodi vide hii tafadhali nitumie ujumbe, nina shilingi elfu 3 zako," Aliandika Amber Ray.