In Summary
  • Terence Creative aadhimisha miaka 4 tangu alipowacha kuvuta sigara
Terence Creative katika studio za Radio Jambo siku ya Ijumaa
Image: RADIO JAMBO

Muunda maudhui  Terence Creative, kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram amefichulia mashabiki wake kwamba ameadhimisha miaka 4 siku 25 tangu aache kuvuta sigara.

Creative alikuwa amevuta sigara kwa miaka 20 kabla ya kuacha, na kufunguka kuhusu uvutaji sigara.

Pia alifichua kwamba anafuraha, kwani anaweza kuwapa ushauri vijana vita dhidi ya tobacco,mwaka jana alisema kwamba alikuwa anavuta pakiti mbili au tatu  za sigara kwa siku moja.

"Sijavuta sigara kwa miaka 4...Ni miaka minne haswa siku 25 tangu niache tumbaku, najisikia furaha kupata kuwatia moyo vijana zaidi katika vita dhidi ya tumbaku, ndio maana natetea #TobaccoTax4Health na @ntakenya." Alisema Creative.

Hizi hapa baadhi ya jumbe za mashabiki;

mburu711: God bless you sir as you continue doing well

dkivango7: Come ladies ofcos will say sigara,if it's a lady ask her btwn make up and uga majority will say uga iongezwe

reden_cartel: God bless you sir as you continue doing well🔥🔥@terencecreative 🙏🙏@reden_cartel

bazenga_wa_muziki_mombasa: @terencecreative Sasa umekuja sana acha kua mtu bladi fucking......tafuta content if you left tobacco it's your own choice....

View Comments