In Summary
  • Msanii Akothee alazwa tena hospitalini siku chache baada ya kuruhusiwa kuenda nyumbani
Image: INSTAGRAM// AKOTHEE

Mwanamuziki mashuhuri wa Kenya Esther Akoth ambaye hujulikana kama Akothee amefichua kwamba alikaa siku ya Jamhuri alikuwa hospotali baada ya kulazwa tena.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram akithibitisha kisa hicho, alipakia picha kadhaa akidai kwamba hakuwa na wakati wa kutumia siku yake ya Jamhuri na familia yake.

Hii Inasemekana ilitokea siku chache baada ya kudaiwa kuruhusiwa kutoka katika hospitali alikokuwa amelazwa kwa muda.

Siku chache zilizopita, Akothee alifichua kuwa alilazwa baada ya kuugua ugonjwa unaojulikana kama ND ambao ni uharibifu wa neva unaosababisha mishipa ya fahamu ya mtu kuhisi ganzi na baada ya hapo inadaiwa kuvimba.

Baada ya kupakia Picha akiwa kwenye kitanda cha hospitali aliandika ujumbe huu;

"Siwezi kuelezea kile kinachonila, lakini kinaendelea kufanya jambo lake kwa wakati mbaya zaidi. Tumekuwa hapa tangu Jumamosi na hii ni sherehe yetu ya jamhuri. Leo naweza kuinua kichwa changu 💪," Akothee Aliandika.

Mashabiki wake walimtumia jumbe huku wakimtakia afueni ya haraka.

View Comments