In Summary
  • Vanessa Mdee amuomboleza ndugu yake
  • Marehemu Adam alikuwa Mkuu wa Majeshi katika ofisi ya Rais mstaafu wa Tanzania Jakaya Kikwete
Vanessa Mdee
Image: Hisani

Msanii kutoka Tanzania Vanessa Mdee kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram amemuombleza ndugu yake mkubwa ambaye aliaga dunia siku 17 zilizopita.

Mdee mwenye hisia alitaja jinsi imekuwa vigumu kwake na familia kukabiliana na kifo kisichotarajiwa cha kaka yake.

Marehemu Adam alikuwa Mkuu wa Majeshi katika ofisi ya Rais mstaafu wa Tanzania Jakaya Kikwete.

“Imepita: siku 17 tangu Happy ampoteze Adam. Siku 17 tangu LJ, Mali na Lamar wampoteze Baba yao. Siku 17 tangu Mama kupoteza mwanawe wa kwanza. Siku 17 tangu G, Nancy, Sam, Mars, Helen, Michael, Noel na mimi tupoteze kaka yetu mkubwa.

Siku 17 tangu Sakry ampoteze mwanamume aliyemtembeza hadi madhabauni siku ya harusi. Siku 17 tangu ABD ampoteze rafiki yake mkubwa. Siku 17 tangu Rais JM Kikwete ampoteze mkuu wake wa kazi. Siku 17 tangu Da Vai ampoteze msiri wake,” Vanessa aliandika.

Mdee alimsifu kaka yake kama mtu mcha Mungu na mkarimu ambaye atakumbukwa na kukumbukwa daima na wapendwa wake.

“Ningeweza kuendelea…kwa sababu ulikuwa mambo mengi sana kwa watu wengi. Na ninapoendelea kupokea rambirambi ambazo siwezi kabisa kuzishughulikia, kuna makubaliano; ‘Adam alikuwa mtu mkubwa sana, mcha MUNGU na mkarimu’.

Hayo ndugu yangu yanasikika kama maisha ya kustaajabisha. Aina ambayo inakufanya uwe mtu wa kutokufa ndani ya mioyo yetu kwa sababu tunakumbuka milele jinsi ulivyotufanya tujisikie 🤍 na huku tukijaribu kuelewa kila kitu na inaumiza kupita kuelewa - tunaendelea. kumshukuru Mwenyezi Mungu."

Aliendelea kunukuu Biblia, Isaya 57:1-2, ambayo inazungumza kuhusu watu wema kufa hata kabla ya wakati wao.

 

 

 

 

View Comments