logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Nimebarikiwa sana kushiriki maisha na wewe,'Joyce Omondi amsherehekea mumewe

Mnamo Desemba 31, mtangazahi huyo alikiri kwamba mwaka wake wa 2021 ulikuwa wa machozi

image
na Radio Jambo

Yanayojiri06 June 2022 - 12:50

Muhtasari


  • Joyce alimtaja Waihiga kama mwanaume aliyekusudiwa kwake akisema kwamba amebarikiwa kushiriki maisha naye

Mwimbaji wa nyimbo za Injili na mtangazaji wa runinga ya Citizen  Joyce Omondi ameandika ujumbe wa kufurahisha kwa mumewe Waihiga Mwaura anapoadhimisha siku yake ya kuzaliwa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Joyce alimtaja Waihiga kama mwanaume aliyekusudiwa kwake akisema kwamba amebarikiwa kushiriki maisha naye.

"Heri ya siku ya kuzaliwa kwa mwanamume wa ndoto zangu na mpenzi wa maisha yangu, #theoneHekeptforme @waihigamwaura ❤️❤️❤️Nimebarikiwa sana kushiriki maisha na wewe. Asante kwa wewe ni nani na yote unayofanya

Hakika wewe ni zawadi inayostahili kusherehekewa kila siku. Kwa hivyo hapa kuna miaka mingi zaidi iliyojaa furaha, upendo, neema na kila kitu kizuri kutoka juu!'' Bi.Omondi aliandika.

Mnamo Desemba 31, mtangazahi huyo alikiri kwamba mwaka wake wa 2021 ulikuwa wa machozi na huzuni nyingi. Alimpoteza babake mnamo Juni, 2021.

"Kusema ukweli, nilitumia muda mwingi wa 2021 nikilia na kuvunjika moyo. Lakini mwaka unapoisha, moyo wangu unajawa na shukurani kwa sababu najua kuwa nimesimama hapa kwa sababu ya neema ya Mungu tu 💯.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved