logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rapa Cardi B ahukumiwa baada ya kukiri mashtaka ya shambulizi katika klabu ya utupu

Mwimbaji huyo allihukumiwa kifungo cha siku 15 katika huduma ya jamii.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri17 September 2022 - 04:41
Rapa huyo alikubali makubaliano ya kukiri siku moja kabla ya kesi yake kusikizwa

Cardi B amekiri makosa mawili yaliyotokana na ugomvi katika klabu ya utupu, kama sehemu ya makubaliano ambayo yanamaanisha kuwa ataepuka kesi na kufungwa jela.

Rapa huyo aliyeshinda tuzo ya Grammy, mzaliwa wa Belcalis Almanzar, alikiri kosa la shambulio la kiwango cha tatu na kusababisha hatari kiwango cha daraja la pili, na alihukumiwa kifungo cha siku 15 katika huduma ya jamii.

Mashtaka mengine kumi yalitupiliwa mbali.

‘’Nimefanya maamuzi mabaya katika siku zangu zilizopita ambayo siogopi kukabiliana nayo na kuyasimamia,’’ alisema katika taarifa.

Mahakamani, kijana huyo mwenye umri wa miaka 29 alikiri kuandaa na kushiriki katika mashambulizi mawili dhidi ya wafanyakazi wa klabu ya usiku ya Angels huko New York mnamo 2018.

Kulingana na mamlaka, matukio hayo yalikua ya ugomvi kati ya Almanzar na dada wawili - mmoja wao aliamini alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mumewe, rapa Offset.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved