logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aliyekuwa muigizaji wa Selina, Lenana Kariba na mkewe mzungu wabarikiwa mtoto wa kwanza

Muigizaji huyo wa zamani wa Selina alifichua kuwa anataka watoto wake wasome nchini Uingereza.

image
na

Habari21 May 2023 - 13:00

Muhtasari


•Huku akitangaza habari hizo njema kwenye mitandao yake ya kijamii; muigizaji huyo alishiriki picha ya binti yake Ava huku akimshika mkono na kuandika.

•Muigizaji huyo wa zamani wa Selina alifichua kuwa anataka watoto wake wasome nchini Uingereza.

Lenana Kariba na mkewe mrembo.

Muigizaji wa Kenya Lenana Kariba na mkewe ni wazazi wapya zaidi mjini baada ya kumpokea mtoto wao wa kwanza.

Huku akitangaza habari hizo njema kwenye mitandao yake ya kijamii; muigizaji huyo alishiriki picha ya binti yake Ava huku akimshika mkono na kuandika.

"Hamjambo wallimwengu..Kutana na Ava   "

Muigizaji huyo wa zamani wa Selina katika kipindi cha Maswali na Majibu kwenye Instagram alifichua kuwa anataka watoto wake wasome nchini Uingereza.

Lenana alifichua kwamba mkewe amekuwa akitamani tufaha na maembe.

Kulingana na Lenana, wanataka kujaribu na kuhakikisha wanapata uzoefu wa maisha katika nchi zote mbili, Kenya na Uingereza.

"....Tutaendelea kusafiri kwenda na kurudi. Shule tunapanga kwenda Uingereza lakini basi, kila likizo tutatoka kwa ndege. Nahitaji wazazi wangu wawafundishe Kikuyu," alisema.

Aliongeza kuwa yuko tayari kufanya bidii katika uzazi na kuwa mwangalifu sana kumpa mtoto wake bora awezavyo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved