Nikitoka Hospitali nitakuwa muhubiri- Peter Miracle Baby aapa
"Bwana asifiwe, nikitoka hapa ntakua pastor, na nitahubiri neno la Mungu," Miracle Baby alisema.
•Miracle Baby ameapa kwamba akitoka hospitali atakuwa mhubiri. Mwanamuziki huyo amekuwa hospitali kwa muda mrefu.
•Mpenzi wake Carol Katrue aliomba mashabiki wao kwenye mitandao ya kijamii wamuweke msanii huyo kwa maombi.
Mwanamuziki wa Gengetone na Mugithi Peter Mwangi anayejulikana kama Peter Miracle baby ameapa kwamba akitoka hospitali atakuwa mhubiri. Mwanamuziki huyo amekuwa hospitali kwa muda mrefu.
"Bwana asifiwe, nikitoka hapa ntakua pastor, na nitahubiri neno la Mungu"
Takriban wiki moja iliyopita alifanyiwa upasuaji wa tatu mnamo Jumanne, Februari 6.
Mpenzi wake Carol Katrue aliomba mashabiki wao kwenye mitandao ya kijamii wamuweke msanii huyo kwa maombi.
"Anaenda kufanyiwa upasuaji wa tatu, tunahitaji maombi yenu," Katrue aliandika kwenye picha ya Miracle baby aliyeonekana akiwa mdhaifu.
Baadaye alieleza mashabiki kuwa upasuaji uliendelea vizuri na akashukuru kila mtu aliyeweka Miracle Baby kwa maombi na kuwaomba wazidi kumwombea.
"Asante Mungu kwa upasuaji uliofaulu lakini endeleeni kumuombea," Katrue aliandika kwa Instagram stories.
Aliendeleza na kueleza kuwa Miracle baby alifanyiwa upasuaji kutokana na kupasuka kwa utumbo.
Siku 2 zilizopita, Katrue aliandika tena kwa mtandao kwamba anaomba mashabiki waoa wawasaidie kukusanya milioni 1.6 ya kulipa bili ya hospitali.