In Summary

• Licha ya kupata muda mfupi, hitmaker huyo wa Samantha aliheshimu kujitolea kwake kutumbuiza kwenye mazishi ya Chira bila malipo yoyote.

Otile Brown
Image: Screengrab

Mwanamuziki Otile Brown ameeleza kutoridhika na muda mfupi aliyopewa jukwaani wakati wa mazishi ya TikToker Brian Chira.

 Otile alisema kwamba alitarajia kupewa muda zaidi kumuomboleza Chira kupitia nyimbo zake. 

"Mbaya sana. Ilikuwa kinyume na matarajio yangu, lakini tutafanya nini?" Alisema.

Licha ya kupata muda mfupi, hitmaker huyo wa Samantha aliheshimu kujitolea kwake kutumbuiza kwenye mazishi ya Chira bila malipo yoyote.

Alipoulizwa kuhusu nia yake, haswa ikiwa alitaka kutangazwa au kuvutia, Otile alikanusha madai hayo.

Alifafanua kuwa uamuzi wake wa kuimba kwenye mazishi hayo ni kitendo cha kumuenzi Chira, shabiki ambaye hakuwahi kukutana naye, akichochewa na wafuasi waliomtaarifu kuhusu kuupenda kwa Chira muziki wake.

"Sionyeshi chochote isipokuwa upendo. Simjui huyo jamaa. Mashabiki waliniletea mawazo kuhusu mtu huyu. Lakini baada ya kwenda kwenye kurasa zake, niligundua kuwa alikuwa shabiki wangu mkubwa. Ikiwa unanijua, utagundua kuwa huwa siendi kwa mazishi ya mtu yeyote. Inafurahisha kwamba watu wangefikiria hivyo. Walitaka nisionekane?” Alisema mwanamuziki huyo.

“Niliona baadhi ya watu wakisema nilipaswa kumuonyesha upendo alipokuwa hai. Kwa hivyo niende kwa kila shabiki sasa na kuonyesha upendo kabla hajakufa?" Otile aliuliza.

Otile alichagua kuimba wimbo wa "One Call" kwenye mazishi ya TikToker baada ya mashabiki kumwambia wimbo huo ndio anaupenda zaidi Chira. Alikuwa amewahimiza waliohudhuria kujifunza maneno ya wimbo huo ili kuimba pamoja na kusherehekea maisha ya Chira.

View Comments