In Summary

•Akiongea kwenye video, nyota huyo wa rap alisema aliwajibika kikamilifu kwa matendo yake kwenye klipu hiyo.

•"Nilichukizwa nilipofanya hivyo. Nimejichukia sasa," alisema katika taarifa yake.

Image: BBC

Sean "Diddy" Combs ameomba msamaha kwa tabia yake "isiyo na udhuru" baada ya CCTV kuonekana kumuonyesha akimshambulia mwimbaji Casandra "Cassie" Ventura.

Akiongea kwenye video iliyotumwa kwenye ukurasa wake wa Instagram, nyota huyo wa rap alisema aliwajibika kikamilifu kwa matendo yake kwenye klipu hiyo.

Kanda hiyo, iliyorushwa hewani na CNN mapema wiki hii, ilionekana kumuonyesha Bw Combs akimpiga teke na kumsukuma mpenzi wake wa zamani kwenye njia ya ukumbi wa hoteli.

"Nilichukizwa nilipofanya hivyo. Nimejichukia sasa," alisema katika taarifa yake. "Nilienda na nikatafuta usaidizi wa kitaalamu.

Niliingia kwenye matibabu, kwenda kituo cha kupata usaidizi. Ilibidi nimuombe Mungu rehema na neema zake. Samahani sana." BBC haijaithibitisha kwa uhuru video hiyo, ambayo inaonekana kuwa ni mkusanyiko wa video za uchunguzi wa tarehe 5 Machi 2016.

Kulingana na CNN, ilirekodiwa katika Hoteli ya InterContinental ambayo sasa imefungwa huko Century City, Los Angeles

View Comments