logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Nilihisi kama atakufa!" Sandra Dacha azungumzia ugonjwa uliokuwa umeathiri Akuku Danger hadi akalazwa ICU

Alisema alilia sana wakati alifika hospitalini na kupata mpenzi wake akiwa amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi kwani alikuwa amelemewa sana.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri29 January 2022 - 07:19

Muhtasari


•Dacha alisema mapafu ya mchekeshaji huyo yalikuwa yamejawa na maji na kuathirika sana kiasi cha kwamba madaktari walisema alihitaji maombi mengi ili kutoka hospitali akiwa hai.

•Alisema alilia sana wakati alifika hospitalini na kupata mpenzi wake akiwa amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi kwani alikuwa amelemewa sana.

Mwigizaji mashuhuri Sandra Dacha almaarufu kama Silprosa amefichua kwamba mpenzi wake mchekeshaji Akuku Danger alikuwa amelazwa hospitalini baada ya kushambuliwa na ugonjwa wa Pneumonia.

Akiwa kwenye mahojiano na Mpasho, Dacha alieleza kwamba ugonjwa huo ulikuwa umeathiri 75% ya mapafu ya Akuku Danger na kumwacha katika hali mahututi.

Dacha alisema mapafu ya mchekeshaji huyo yalikuwa yamejawa na maji na kuathirika sana kiasi cha kwamba madaktari walisema alihitaji maombi mengi ili aweze kutoka hospitali akiwa hai.

"Pneumonia ilikuwa imekula 75% ya mapafu yake, ilikuwa imebaki 25%. Asilimia 75 ni kubwa. Alikuwa na pneumonia na ndio maana alikuwa na matatizo ya kupumua. Madaktari walishinda wakitwambia maombi ni muhimu. Maji ilikuwa imejaa kwa mapafu. Ilikuwa kati yake  na Mungu, ni Mungu" Dacha alisema.

Mwigizaji huyo alisema alifahamishwa kwamba Akuku Danger anaugua mnamo mkesha wa mwaka mpya.

Dacha alisema alilia sana wakati alifika hospitalini na kupata mpenzi wake akiwa amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi kwani alikuwa amelemewa sana.

"Ilikuwa mbaya. Nilihisi kama kwamba angekufa. Madaktari walikuwa wanasema tuombe Mungu. Lakini Mungu ni nani, amepona" Dacha alisema.

Dacha amehakikishia mashabiki kwamba afya ya Akuku Danger imeimarika na tayari ameruhusiwa kwenda nyumbani.

Hata hivyo amewasihi kuendelea kuchanga kwani bado hawajakamilisha kulipa bili ya hospitali. Amesema walikubaliana na usimamizi wa hospitali kwamba salio lingelipwa ndani ya kipindi cha wiki tatu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved