logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Harmonize ameishiwa hela, wandani wake wanaondoka?

Baba Levo aliandika ujumbe ulionekana kuelekezwa kwenye kambi la Konde Gang

image
na

Habari09 February 2022 - 11:46

Muhtasari


•Baada ya habari za H-baba kusambaa  kwenye mitandao ya kijamii akiwa anamsifia mwanamuziki nguli wa Bongo Fleva, Diamond platnumz.

• Babalevo alieleza kwamba kazi aliyokuwa amepewa na bosi wake, ameifanya kwa ukamilifu kama alivyoagizwa naye

Baba Levo na Harmonize

Baada ya habari za H-baba kusambaa  kwenye mitandao ya kijamii akiwa anamsifia mwanamuziki nguli wa Bongo Fleva, Diamond platnumz.

Mwandani wa Diamond, Babalevo kupitia ukurusa wake instagram ameandika ujumbe ambao ulionekana  kuelekezwa kwenye Kambi ya Konde Gang.

Kulingana na kauli yake, alieleza kwamba kazi aliyokuwa amepewa na bosi yake, ameifanya kwa ukamilifu kama alivyoagizwa naye.

“Bosi nimemaliza kazi,wamegundua kwamba  ukweli kwamba ‘Kilandage’ hana hela angewaua na njaa, ombi langu kwako wapokee kwa upendo kisha wape kazi wapate pesa maisha yaendelee. Ni vijana wenzetu,” aliandika Babalevo.

Kauli hii imetafsiriwa na wafuasi wa Babalevo kwamba anawakaribisha wanaohamia Wasafi kutoka KondeGang.

Ikumbukwe ni mwezi jana tu ambapo msanii Country Boy aliondoka kwenye lebo ya KondeGang, wa hivi karibuni anayekisiwa kuondoka akiwa  mwandani wa Harmonize ,H-baba.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved