logo

NOW ON AIR

Listen in Live

BASATA yawapiga WCB Wasafi kifaa butu kichwani

BASATA imewatema wasanii wote kutoka WCB Wasafi kuwania Tanzania Music Awards.

image
na Radio Jambo

Habari21 March 2022 - 04:17

Muhtasari


• Baraza la sanaa Tanzania (BASATA) limewatema wasanii wote kutoka WCB Wasafi nje ya orodha ya kuwania tuzo za Tanzania Music Awards.

Wikendi iliyopita kumekuwa na maneno mengi mitandaoni yenye hisia kinzani baada ya baraza la sanaa Tanzania, BASATA kutoa orodha ya wasanii watakaowania tuzo katika vitengo mbalimbali.

Minong’ono hiyo imetokana na kwamba katika orodha hiyo, hakuna msanii hata mmoja kutoka rekodi lebo ya WCB Wasafi ambaye ameorodheshwa.

Kulingana na mabango ya BASATA ya orodha hiyo ambayo wameipakia kwenye instagram yao, wasanii wengi tu tena nguli kutoka nje ya Wasafi wametajwa mule lakini wale wenye uswahiba na Wasafi, wakiwemo Rayvanny na msanii wake MacVoice kutoka Next Level Music wamezimiwa taa za mchana.

Wasanii kama vile Alikiba, Harmonize, Nandy, Juma Jux, Marioo ni baadhi ya majina tajika ambyo yameonekana kwenye orodha ya kuwania Tanzania Music Awards katika vipengele tofauti tofauti.

Kukosekana kwa wasanii wa Wasafi kunatajwa kutokana na msanii Diamond Platnumz kutofautiana wazi na BASATA kwa kusema kwamba hajawahi nufaika na marupurupu yanayotolewa na baraza hilo kwa wasanii.

Diamond pia alilalamikia hatua ya muigizaji Steven Nyerere kuteuliwa kuwa msemaji na mratibu wa mipango wa wasanii kwa kile alikitaja kuwa hakufaa kwa sababu yeye si msanii wa bongo fleva.

Bila shaka hii ni vita kati ya rekodi lebo ya Wasafi na baraza la Sanaa ambapo kwa mara ya kwanza katika tukio hili ambalo si la kawaida, wasanii wote wa Wasafi hawatawania tuzo yoyote katika Tanzania Music Awards.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved