logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Baba Levo: Daimondi akifa nitalia kuliko Zuchu

Baba Levo - Daimondi akifa nitalia kuliko Zuchu..!! maana tangu ameanza kunisaidia maisha yangu yamebadilika

image
na Radio Jambo

Habari25 March 2022 - 14:35

Muhtasari


Daimondi akifa nitalia kuliko Zuchu..!! maana tangu ameanza kunisaidia maisha yangu na watoto wangu yamebadilika kabisa..!! maana tangu ameanza kunisaidia maisha yangu na watoto wangu yamebadilika kabisa

Baba Levo na wasanii Diamond na Zuchu

Msanii mwenye utata mwingi kutokea bongo Tanzania, Baba Levo amezua mapya kabisa ambayo yamelichemsha gumzo zito kuhusu uwezekano wa Diamond Platnumz kuwa katika mahusiano na Zuchu.

Baba Levo ameandika ujumbe wenye ukakasi kwenye Instagram yake akisema kwamba Diamond akifa atabubujikwa zaidi na machozi kuliko msanii Zuchu ambaye kwa siku za hivi karibuni ameonekana kuwa na ukaribu usio wa kawaida na bosi wake Diamond Platnumz.

Baba Levo aidha hajaweka wazi kama anamtakia Diamond kifo au vipi lakini amefafanua kwa kiduchu tu kwamba kulia kwake kwa wingi mpaka kushinda taji na muombolezaji ‘bora’ zaidi ya mtu yeyote yule ni kwa sababu ya heshima zake kwa Simba ambaye alimsaidia na kumuaminia wakati hakuna mtu alitaka kufanya kazi na yeye.

“Daimondi akifa nitalia kuliko Zuchu..!! maana tangu ameanza kunisaidia maisha yangu na watoto wangu yamebadilika kabisa. thanks @diamondplatnumz mungu akuongezee ..! tunakuombea sana..!” Aliandika Baba Levo kwenye Instagram yake.

Wengi wameonekana kutoelewa pointi ya Baba Levo hapa huku baadhi wakidai kwani ukiwa unamheshimu mtu mpaka umtakie kifo ili uje kudhihirisha heshima hizo wakati wa msiba wake.

Sijui wewe unalitafakari vipi hili!


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved