logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Yuko 'broke' hana pesa,'Ringtone asema huku akisisitiza anayajua mengi kuhuru Eric Omondi

Eric Omondi bado hajajibu video yake inayosambaa mtandaoni

image
na Radio Jambo

Habari02 May 2022 - 08:24

Muhtasari


  • Ringtone hatimaye amekiri kwamba Eric Omondi anaishi maisha duni na kwamba hana pesa

Mcheshi Eric Omondi alivuma sana wikendi iliyopita baada ya kuwa kwenye drama isioeleweka na staa wa bongo wa Tanzania Harmonize.

Wawili hao walikejeliwa sana mitandaoni na wanamitandao,uku drama hiyo ikimsababishia Harmonize kukamatwa na kuzuiliwa katika kituo cha polisi cha Kileleshwa.

Ringtone hatimaye amekiri kwamba Eric Omondi anaishi maisha duni na kwamba hana pesa.

Ringtone kwenye mahojiano alisema kuwa Erick ana deni na pia aliongeza kuwa ametuma maombi yote ya mkopo kutoka kwa programu mbalimbali za maombi ya mkopo ikiwa ni pamoja na Tala.

Eric Omondi bado hajajibu video yake inayosambaa mtandaoni lakini ni dhahiri kwamba atafanya hivyo bila muda.

Ringtone Apoko pia badala yake anamfahamu Eric Omondi zaidi na hata marafiki zake.

Eric Omondi amekuwa akitoa wito kwa vyombo vya habari kucheza muziki wa Kenya, huku akifanya kazi nyuma ya pazia na Harmonize ili kukuza muziki wa Tanzania.

Siku ya JUmapili Eric alidai kwamba baada ya kuenda kumtembelea Harmonize polisi alimchapa ngumi.

Pia aliyekuwa gavana wa kaunti ya Nairobi Mike Sonko alisema kwamba hakumshtaki staa huyo.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved