logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Juju haikukaa sana kwangu!" Aliyekuwa mpenzi wa Amber Ray amshtumu kwa kutumia uchawi

"Asante Mungu kwa kunisaidia" Kabba amesema.

image
na Radio Jambo

Habari07 May 2022 - 08:21

Muhtasari


•IB Kabba amemshtumu mama huyo wa mtoto mmoja kwa kumfanyia uchawi wakati wa mahusiano yao ya muda mfupi.

•Kabba  amewasihi wanaume kuwa makini zaidi na wanawake wanaochumbiana nao huku akidai kuwa baadhi yao ni hatari.

Amber Ray na aliyekuwa mpenzi wake IB Kabba

Mchezaji mpira wa vikapu kutoka Sierra Leone IB Kabba amethibitisha kuwa hayupo tena kwenye mahusiano na mwanasoshalaiti Amber Ray.

Amber Ray alimtambulisha mwanariadha huyo kwa wanamitandao mwezi Februari ila baada ya kipindi kifupi mahusiano yao yakagonga mwamba.

IB Kabba sasa anamshtumu mama huyo wa mtoto mmoja kwa kumfanyia uchawi wakati wa mahusiano yao ya muda mfupi.

"Mimi ni mtu huru kama Mandela. Juju haikukaa sana kwangu. Asante Mungu kwa kunisaidia," IB Kabba amesema kupitia Instagram.

Hapo awali IB Kabba alikuwa amedokeza kuwa mahusiano yake ya kipindi kifupi na Amber Ray yalikuwa 'sumu.'

"Amepindishwa kila kitu, kwanini nitake kudhibiti maisha yake? Alikuwa akitumia simu yangu na ku-block watu kwenye Instagram na sijawahi kuingia kwenye simu yake. Nilichokuwa najaribu kujenga na alichokuwa anajaribu kukifanya, Ujenzi ulikuwa tofauti. Haikufaulu." Kabba alisema kwenye mahojiano.

Kabba  amewasihi wanaume kuwa makini zaidi na wanawake wanaochumbiana nao huku akidai kuwa baadhi yao ni hatari.

"Tuwe makini na baadhi ya wanawake ambao watakuja katika maisha yetu, simdharau mwanamke yeyote, ninawaheshimu wanawake na nitawapenda milele lakini daima tuwe makini na kupata wanaofaa. Mungu akubariki," Kabba aliandika kwenye Instastori zake.

Hivi majuzi Amber Ray aliweka wazi kuwa yupo single baada ya kutengana na IB Kabba.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved