logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Wakati wa kunipa block ni huu,'Amber Ray kwa wasio mpenda

Pia aliwaambia kwamba wakati huu hawatamuweza.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri10 May 2022 - 13:12

Muhtasari


  • Mwanasosholaiti Amber Ray amekuwa akivuma kwa muda kwenye mitandao ya kijamiim kwa ajili ya maisha anayoishi

Mwanasosholaiti Amber Ray amekuwa akivuma kwa muda kwenye mitandao ya kijamiim kwa ajili ya maisha anayoishi.

Siku ya Jumanne kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram amewashauri wote ambao wanamchukia waweze kumpa block au kuacha kumfuata mitandaoni.

Pia aliwaambia kwamba wakati huu hawatamuweza.

"Masaa ni ya kununua pressure pills na painkillers,juu Weh 🤣🤣 hamtaniweza round hii…. Na Wasio nipenda Wakati wa kuni unfollow ndio huu pia… in fact, just block me!🤣🥳," Amber Aliandika.

Amber Ray anasema itabidi ampe bintiye masomo ya jinsi ya kupenda lakini muhimu zaidi ni wakati gani wa kuacha kupenda.

Mama wa mtoto mmoja anasema hakuwahi kufundishwa jinsi ya kuacha kupenda, lakini tu jinsi ya kupenda watu.

Amber anasema hataki binti yake apate uchungu ambao amekuwa nao kwa kupenda watu bila kikomo.

Nitamfundisha binti yangu jinsi ya kupenda, lakini muhimu zaidi jinsi ya kuacha. Sikufundishwa jinsi ya kuacha ..... Ilinibidi kujifunza mambo hayo kwa bidii. ! #amberthebrand," Amber Ray aliandika.

Mashabiki wa Amber Ray walitoa maoni yao kuhusu chapisho lake wakisema wanamsubiri mtoto wa kike.

Kwa wengine, hili lilikuwa dokezo kwamba anaweza kupata mtoto hivi karibuni.

Ingawa Amber anazungumza kuhusu kile atakachomfundisha binti yake, mapema mwaka jana alisisitiza kwamba hataki kupata mtoto mwingine.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved