logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Pritty Vishy apingana na ex wake Stivo Simple Boy kuhusu suala la ngono kabla ya ndoa

•Vishy amesema kuwa wapenzi wanafaa kufurahia tendo la ndoa hata kabla ya kufunga pingu za maisha. •Stivo alifichua kuwa yeye bado ni bikra na kwa kuwa hataki kukiuka agizo la Biblia linalosema watu hawapaswi kushiriki ngono kabla ya ndoa.

image
na Radio Jambo

Habari24 May 2022 - 07:02

Muhtasari


•Vishy amesema kuwa wapenzi wanafaa kufurahia tendo la ndoa hata kabla ya kufunga pingu za maisha.

•Stivo alifichua kuwa yeye bado ni bikra na kwa kuwa hataki kukiuka agizo la Biblia linalosema watu hawapaswi kushiriki ngono kabla ya ndoa.

Stivo Simple Boy na aliyekuwa mpenzi wake Pritty Vishy

Purity Vishenwa almaarufu Pritty Vishy amepingana na maoni ya aliyekuwa mpenzi wake Stivo Simple Boy kuhusu suala la watu kushiriki mchezo wa kitandani kabla ya ndoa. 

Vishy amesema kuwa wapenzi wanafaa kufurahia tendo la ndoa hata kabla ya kufunga pingu za maisha.

"Watu wasingoje. Hata ukienda kunua gari, lazima ujaribu ingini kama inafanya kazi," Vishy alisema katika mahojiano na SPM Buzz.

Hisia za Vishy kuhusu suala hilo zinapingana na zile za Stivo Simple Boy ambaye hivi majuzi alisema watu wanafaa kufunga ndoa kabla ya kushiriki mapenzi.

Stivo alifichua kuwa yeye bado ni bikra na kwa kuwa hataki kukiuka agizo la Biblia linalosema watu hawapaswi kushiriki ngono kabla ya ndoa.

"Mapenzi yanafaa kufanywa kama mtu ameoa ama ameolewa. Sio mambo ya kucheza cheza hapa na pale alafu msichana akishapata mimba  jamaa anatoroka. Hiyo haifai. Sijawahi kufanya mapenzi kwa kuwa bado sijaoa," Stivo alisema katika mahojiano na Eve Mungai.

Mwanamuziki huyo kutoka Kibra alidokeza kuwa mahusiano yake na Vishy yalifika kikomo baada ya kipusa huyo kusisitiza washiriki mapenzi, jambo ambalo hakukubaliana nalo kwa kuwa hawakuwa kwenye ndoa rasmi.

Alisema kuwa msimamo wake wa kukataa kushiriki mapenzi haukumfurahisha Vishy na ndiposa akaamua kumtema.

"Yeye hakutaka  kusikia. Alisema Simple Boy ameokoka sana ni heri aende kwa mwingine. Nilikataa," Alisema.

Vishy ameweka wazi kuwa sasa yupo single ila bado hayupo tayari kujaribu mahusiano mengine kwa sasa.

"Natafuta mchumba. Lakini wasianza kunitafuta saa hii. Wacheni kwanza nitafute pesa ata mimi," Alisema.

Vishy na Stivo walithibitisha kutengana kwao takriban miezi miwili iliyopita. Wakati huo Vishy alimshtumu mpenzi huyo wake kwa kumcheza na mwanadada mwingine.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved