logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Shakilla ajiunga na App ya kuchumbiana katika harakati za kujitafutia mwanamume

Aidha mwanasosholaiyti huyo alikiri kwamba hawezi chumbiana na wanaume Wakenya.

image
na Radio Jambo

Makala08 February 2023 - 12:46

Muhtasari


  • Ufichuzi huo hata hivyo unajiri takriban wiki mbili baada ya Shakilla kutumia akaunti yake ya Instagram kutangaza masikitiko yake

Mwanasosholaiti mwenye utata Shakilla  leo amefichua kwa mashabiki wake kwamba amejiunga rasmi na programu ya kuchumbiana ya Tinder.

Alifichua haya kupitia kwenye insta stories zake, ambapo alisema kuwa lengo lake kuu lilikuwa hatimaye kujipatia mwanamume ambaye anatumai atakuwa kwenye uhusiano naye.

“Lazima nitafute mwanamume kwa vyovyote vile” aliandika Shakilla.

Ufichuzi huo hata hivyo unajiri takriban wiki mbili baada ya Shakilla kutumia akaunti yake ya Instagram kutangaza masikitiko yake.

Hii ni kwa sababu hakuna hata mmoja wa wafuasi wake wa kiume kwenye mitandao ya kijamii aliyeonyesha nia ya kutaka kuchumbiana naye.

Kupitia hadithi zake za insta, msichana huyo wa miaka 22 alilalamika kwamba hakuna mwanamume aliyemkaribia kwa uhusiano wa dhati.

Shakilla alizidi kujiuliza kama alikusudiwa kuwa single milele.

"Wafuasi wangu wote hakuna anayetaka kuingia katika uhusiano wa dhati nami. Je, nilikusudiwa kuwa mtaani maishani" Shakilla aliandika.

Aidha mwanasosholaiyti huyo alikiri kwamba hawezi chumbiana na wanaume Wakenya.

"Wanigeria ndio watu watamu zaidi unaoweza kukutana nao wanakupa pesa na kukutendea vyema. Siwezi kamwe kuchumbiana na mvulana Mkenya. Mimi si Mkenya kwa hivyo nina haki ya kufanya hivyo," Shakilla alisema wakati wa kipindi cha moja kwa moja cha Instagram.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved