logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Vera Sidika azungumzia mipango ya harusi yake

Kwa sasa Vera ana wafuasi zaidi ya milioni mbili kwenye akaunti yake ya ukurasa wa Instagram.

image
na Radio Jambo

Makala26 February 2023 - 07:09

Muhtasari


  • Vera amefichua kuwa sababu ya yeye kuchukua muda wake ni kutaka kufanya moja ya harusi kubwa Afrika Mashariki

Vera Sidika ni mmoja wa watu mashuhuri nchini Kenya. Vera amekuwa kwenye tasnia ya umaarufu kama mtu mashuhuri kwa zaidi ya miaka kumi.

Kwa sasa Vera ana wafuasi zaidi ya milioni mbili kwenye akaunti yake ya ukurasa wa Instagram.

Vera kwa sasa ameolewa na Brown Mauzo na wamezaa mtoto mmoja pamoja na mwingine yuko njiani anakuja kwani Vera ni mjamzito.

Brown na Vera hawakufanya harusi kubwa ya kanisa.

Vera na Brown walifanya harusi fupi ya kiserikali katika ofisi ya mwanasheria Mkuu ambapo wawili hao walibeba mashahidi wachache tu.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram Vera amefunguka kuwa mipango inaendelea na hivi karibuni anapanga kufunga ndoa kubwa na Brown Mauzo.

Vera amefichua kuwa sababu ya yeye kuchukua muda wake ni kutaka kufanya moja ya harusi kubwa Afrika Mashariki.

Mwanasosholaiti huyo alifichua haya baada ya mmoja wa mashabiki kumuuliza'

"Bado unairikiria kufanya harusi kanisani?"

Vera alijibu na kusema;

"Ndio kwa mapenzi ya Mungu itakuwa harusi kubwa kuwahi onekana Afrika mashariki."

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved