logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Huddah Monroe akubali kuwa na mke mwenza atakapoolewa

Huddah alisema  kuwa atamruhusu mumewe mtarajiwa kuoa mke wa pili.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri01 August 2022 - 05:50

Muhtasari


•Mwanasosholaiti hata hivyo alidokeza kuwa ni sharti  mwanaume awe na pesa za kutosha kabla ya kuoa mke mwingine.

Mwanasosholaiti Huddah Monroe

Huddah Monroe amekiri kuwa yuko tayari kuwa katika ndoa ya wake wengi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Huddah alisema  kuwa atamruhusu mumewe mtarajiwa kuoa mke wa pili.

Mwanasosholaiti hata hivyo alidokeza kuwa ni sharti  mwanaume awe na pesa za kutosha kabla ya kuoa mke mwingine.

'Sijali mume wangu kuoa mke wa pili ikiwa ni tajiri na anaweza kututunza, kwa sababu sifikirii kumhudumia mume wangu kwa maisha yangu yote,'' Huddah alisema.

Kwa kawaida, mwanasoshalaiti huyo  huwa haogopi kusema anachofikiria au kutangaza matamanio yake.

Monroe huwa hajali  maoni ya watu kuhusu kile anachochapisha kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii.

Huku hayo yakisemwa, Huddah huwafahamisha wafuasi wake kuhusu kile anachofikiria kuhusu maisha yake.Siku za hivi majuzi amekuwa akiangazia masuala ya ndoa.

''Wakati fulani nitakuwa nimechoka, na atakuwa mzee pia, kila mmoja anachoka  kadri muda unaposonga'' Huddah alisema.

Kwa sasa hakuna yule ambaye ana ukweli wa mambo kuhusu mahusiano ya mwanasosholaiti  huyo.

Inadaiwa kuwa yupo  kwenye mahusiano na mkali wa muziki wa RnB kutoka Bongo, Juma Musa Mkambala almaarufu Juma Jux .

Lakini Jux aliweka wazi kuwa yeye na Huddah ni marafiki tu na hakuna uhusiano yoyote kati yao.

Huddah ambaye sasa amefikisha mwaka thelathini anajifurai maisha yake ya ukapera akijipa moyo kuwa kuna siku naye pia ataolewa na kufurahia ndoa yake.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved