logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Karen Nyamu ashtumiwa kumfuata Samidoh Australia kumzuia asipate mpango wa kando, ajibu

Karen na Samidoh wamekuwa wakifurahia muda pamoja nchini Australia katika siku kadhaa za hivi majuzi.

image
na Radio Jambo

Makala14 September 2023 - 12:13

Muhtasari


•Shabiki alidai sababu pekee iliyomfanya mwanasiasa huyo kujiunga na Samidoh nchini Austaralia ilikuwa kulinda mipaka yake.

•“Side dish tunakuanga kanairo. Sasa ni mwanaume mgani anataka sidefish wa mbali hivyo,” Karen Nyamu alijibu.

Senetor Karen Nyamu alitoa jibu la kejeli baada ya mwanamtandao kumshutumu kwa kumfuata mpenzi wake Samidoh hadi nchini Australia ili kumzuia kutafuta mpenzi mwingine katika taifa hilo la bara Oceania.

Karen na Samidoh wamekuwa wakifurahia muda pamoja nchini Australia katika siku kadhaa za hivi majuzi. Mwimbaji huyo wa Mugithi alifanya ziara ya kikazi nchini humo mapema mwezi huu na seneta huyo wa UDA akajiunga naye huko siku chache baadaye na hata kujiunga naye kwenye matamasha yake ya muziki.

Katika moja ya machapisho yake ya Karen kwenye mitandao ya kijamii siku ya Alhamisi, mtumiaji wa Instagram alidai kwamba sababu pekee iliyomfanya mwanasiasa huyo kujiunga na Samidoh nchini Austaralia ilikuwa kulinda mipaka yake.

"Alienda kuchunga bwana wa wenyewe asichukue another side chick.. Karen uko na kibarua," @dorcaskagwi aliandika chini ya post ya Instagram ya Karen.

Katika jibu lake, mama huyo wa watoto watatu alibainisha kwamba hakuna mwanaume ambaye hutafuta mpango wa kando katika nchi ya mbali.

“Side dish tunakuanga kanairo. Sasa ni mwanaume mgani anataka sidefish wa mbali hivyo,” Karen Nyamu alijibu.

Samidoh amekuwa akiwaburudisha mashabiki wake nchini Australia katika siku kadhaa zilizopita na mama wa watoto wake wawili amekuwa akionekana naye mara kwa mara.

Siku ya Jumatano jioni, Karen alishiriki video zao wakipelekwa na taxi kwenye nyumba moja iliyo msituni ambako walilala. Katika video hizo, wawili hao walionekana wakiburudika pamoja na hata kutaniana mara kwa mara walipokuwa wakienda nyumbani.

Kulikuwa na tukio la kusisimua ambapo seneta huyo wa kuteuliwa alimuuliza Samidoh kama anaweza kujisaidia haja ndogo nje msituni.

“Babe naweza kukokojoa hapa? Karen alimuuliza mzazi mwenzake.

Mwimbaji huyo wa nyimbo za Mugithi hata hivyo kwa utani alimzuia mpenzi huyo wake dhidi ya kufanya hivyo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved