logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Harmonize afunguka kuhusu kukamatwa kwake Zanzibar

Konde Boy alithibitisha alitiwa mbaroni kwa kusababisha usumbufu wakati wa kipindi kitakatifu.

image
na Radio Jambo

Habari11 May 2023 - 03:57

Muhtasari


•Katika taarifa yake, mwimbaji huyo alifichua ataachia kibao hicho Ijumaa na kujigamba kuwa ni cha aina yake kuwahi kufanywa.

•Alitoa shukrani kwa Baraza la Sanaa la Zanzibar kwa kufikia makubaliano naye ambapo alitozwa faini na kuachiliwa huru.

Staa wa Bongo Rajab Abdul Kahali almaarufu Harmonize amefichua kuwa ametayarisha kibao maalum kwa kisiwa cha Zanzibar, nchini Tanzania.

Katika taarifa yake ya Jumatano jioni, mwimbaji huyo alifichua ataachia kibao hicho Ijumaa na kujigamba kuwa ni cha aina yake kuwahi kufanywa.

"Tangu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanza hata kabla ukimpata msanii aliyeimba wimbo unaoitwa Zanzibar noo nikupatie m5 kama zawadi!! Awe ametokea bara ama visiwani!!Licha ya umaarufu wake wote duniani ukijumlisha na kuwa inapokea mamilioni ya watalii kutoka mataifa mbalimbali Africa na kote duniani, huu ndio unaenda kuwa wimbo wao wa Zanzibar," Harmonize alisema kwenye Instastori zake.

Bosi huyo wa Kondegang alidokeza kuwa anatarajia wimbo kupendwa sana hasa visiwani Zanzibar na utachezwa vilabuni vyote.

Wakati huohuo, alifunguka kuhusu kipindi alipokamatwa katika kisiwa hicho kizuri wakati wa msimu wa Ramadhan. Alithibitisha kwamba alitiwa mbaroni kwa kusababisha usumbufu wakati wa kipindi kitakatifu.

"Hata mimi nilikuwa nafunga. Makelele na ibada haviendani kabisa. Ukichanganya na mihangaiko ya hapa na pale jua linapiga tunastahili kabisa kusimamishwa," alisema.

Staa huyo alitoa shukrani za dhati kwa Baraza la Sanaa la Zanzibar kwa kufikia makubaliano naye ambapo alitozwa faini na kuachiliwa huru.

Hata hivyo alidokeza kuwa alifanya wimbo huo kwa ajili ya nchi yake ya Tanzania na wala si kwa manufaa yake binafsi.

"Najua kupitia wimbo huu Zanzibar haitonisahau milele. Hata nikisahaulika mimi hii sauti itabaki vichwani mwa Watanzania wote na yeyote atoke kujanya Zanzibar au hata ukiiwaza Zanzibar,"  Harmonize alisema.

Konde Boy aliwataka mashabiki wake kusubiri kibao hicho siku ya Ijumaa,Mei 12, ambapo atakiachia.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved