logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond azungumzia suala la Zuchu kumweka kwenye wallpaper ya simu yake

Alisema kuwa hilo ni jambo la kawaida na haimaniishi kwamba wako kwenye mahusiano.

image
na Radio Jambo

Makala15 March 2022 - 03:08

Muhtasari


• Diamond alisema kuwa hatua hiyo iliashiria kuwa Zuchu anathamini kazi yake kama bosi wake katika WCB.

•Staa huyo ambaye hivi majuzi aliachia EP mpya 'FOA' aliweka wazi kuwa yeye amesave Zuchu kama 'Zuu' kwenye simu yake.

Diamond Platnumz na Zuchu

Bosi wa WCB Diamond Platnumz amefurahia hatua ya msanii wake Zuchu kumsave kwa jina tamu kwenye simu yake na kuweka wallpaper ya picha yake.

Akiwa kwenye mahojiano na Wasafi Media, Diamond alisema kuwa hatua hiyo iliashiria kuwa Zuchu anathamini kazi yake kama bosi wake.

Diamond alisema kuwa hilo ni jambo la kawaida na haimaniishi kwamba wako kwenye mahusiano.

"Unapokuwa kiongozi unahifadhiwa kwa majina tofauti. Mimi kama kiongozi wake wa taasisi, hakuna ubaya yeye kuniweka katika DP. Kama kweli alikuwa ameniweka, nami nafaa nimshukuru sana. Inaonyesha anathamini juhudi ambazo naweka  katika taaluma yake," Diamond alisema.

Staa huyo ambaye hivi majuzi aliachia EP mpya 'FOA' aliweka wazi kuwa yeye amesave Zuchu kama 'Zuu' kwenye simu yake.

Zuchu alipokuwa katika studio za Wasafi mwezi jana picha za Diamond zilionekana kwenye wallpaper ya simu  yake.

 Wakati ule alisisitiza kuwa hatua yake hakikumaanisha kuwa ana hisia za kimapenzi kwa bosi wake Diamond Platnumz.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved