logo

NOW ON AIR

Listen in Live

King Kaka azungumzia kutopromote album ya Arrow Bwoy

King Kaka amezungumzia kutopost album ya Arrow Bwoy akisema anamtakia mema.

image
na Radio Jambo

Makala15 March 2022 - 05:25

Muhtasari


• Alisema kwamba amekuwa akisafiri, hivyo kukosa muda wa kuisikiliza album hiyo.

• King Kaka aliweka wazi kwamba hakuna tofauti zozote kati yake na Arrow Bwoy.

Rapa matata kutoka humu nchini, King Kaka hatimaye amefunguka kuhusu kitendo chake cha kutopost na kusambaza album ya Arrow Bwoy.

Akizungumza katika mahohiano na mwanablogu 2mbili, King Kaka alisema kwamba hakuna ugomvi wowote na msanii huyo na kukiri kwamba anamtakia kila la kheri katika safari yake ya muziki.

King Kaka alisema kwamba amekuwa na safari za mara kwa mara katika mataifa ya ughaibuni kwa hivyo hajapata muda kuisikiliza album hiyo na kuahidi kwamba atatenga muda na kuzichambua nyimbo kwenye album ya Arrow Bwoy.

"Nimekuwa na safari za hapa na pale lakini nikitulia nitasikiliza album yake," King alisema.

Mwanamuziki huyo alidokeza kwamba Arrow ni msanii anayejituma katika kazi zake na kwamba atazidi kufanikiwa katika chochote anachokifanya.

Ifahamike kwamba kipindi cha nyuma Arrow Bwoy  alikuwa amesajiliwa chini ya lebo ya Kaka Empire inayomilikiwa na King Kaka.

Pia aliwataka mashabiki kumpa sapoti Arrow Bwoy na kununua muziki wake kuutoka kwa album ya #Focus.

Kulingana na Arrow, alihisi kwamba ulikuwa wakati mwafaka wa kutanua mbawa zake na kujisimamia mwenyewe katika kazi zake za muziki.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved