logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nadia Mukami abubujikwa na machozi akisimulia huzuni iliyomkumba baada ya kupoteza mimba

Amesema alijaribu sana kuficha hisia zake na kujifanya kama kwamba yupo sawa.

image
na Radio Jambo

Habari28 March 2022 - 19:49

Muhtasari


•Mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 25 aliwezwa na hisia alipokuwa anafunguka yaliyojiri wakati ujauzito wake uliharibika.

•Katika kipindi hicho, mama huyo wa mtoto mmoja alijaribu sana kuficha hisia zake na kujifanya kama kwamba yupo sawa.

Malkia wa muziki wa kisasa, Nadia Mukami amefichua kwamba alipoteza ujauzito wake wa kwanza mnamo Aprili 12, 2021.

Mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 25 aliwezwa na hisia alipokuwa anafunguka yaliyojiri kupitia Youtube Channel yake.

Nadia alifichua kwamba alikumbwa na kiwewe kikubwa kutokana na tukio hilo la kutisha  hadi kulazimika kupata ushauri wa kisaikolojia.

"Ulikuwa wakati mgumu kuwahi pitia. Huo ndio wakati nilitamani singekuwa msanii. Hospitalini nilioshwa, nilipotoka bado nilikuwa na trauma. Nilipitia kiwewe hadi nikaenda kupata ushauri. Nilikuwa naenda kupata ushauri na watu hawakujua, huo ndio wakati nilikuwa natengeneza ofisi yangu. Nilishauriwa sana na ilisaidia sana," Nadia alisimulia.

Katika kipindi hicho, mama huyo wa mtoto mmoja alijaribu sana kuficha hisia zake na kujifanya kama kwamba yupo sawa.

"Kila mtu alikuwa ananiangalia kama kielelezo, hakuna aliyejali matatizo yangu. Hiyo ndio sababu nilijichagua mimi. Nimeamua kuwa mkweli kadri iwezekanavyo. .. nimepigana sana mwaka uliopita. Kama kuna mtu amejua kujiekelea vitu ni mimi. Nilipoteza marafiki wengi 2021 kwa sababu sikuwa na wakati wa kujieleza," Alisema.

Msanii huyo hata hivyo alibahatika kupata ujauzito mwingine takriban miezi miwili baada ya kupoteza ule wa kwanza. Alijifungua mtoto wa kiume mnamo Machi 4.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved