logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(+Video) Akothee awezwa na hisia huku akiwaona watoto wake baada ya miezi 8

Akothee amesema watoto wake ndio zawadi kubwa zaidi amewahi kupokea maishani.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri09 April 2022 - 11:47

Muhtasari


•Akothee aliwapokea Fancy Makadia, Prince Ojwang na Prince Oyoo katika uwanja wa ndege Jumamosi asubuhi .

•Mama huyo wa watoto watano alisema watoto wake ndio zawadi kubwa zaidi amewahi kupokea maishani.

Akothee na familia yake

Hatimaye mwanamuziki na mjasiriamali Esther Akoth almaarufu kama Akothee anaweza kufurahia wakati na familia yake yote baada ya watoto wake watatu wa mwisho kurejea nchini.

Akothee aliwapokea Fancy Makadia, Prince Ojwang na Prince Oyoo katika uwanja wa ndege Jumamosi asubuhi kwa shangwe kubwa. Alikuwa ameandamana na mpenzi wake Nelly Oaks pamoja na mabinti wake wakubwa Vesha Okello na Rue Baby.

Mama huyo alipakia video akiwapokea watoto hao wake na kusema imekuwa miezi minane tangu mara ya mwisho kuonana nao uso kwa uso.

"Imekuwa miezi 8. Ni muda mrefu sana kusubiri wakati huu. Mungu awatie nguvu wazazi wote wanaofanya kazi mbali na familia zao ili kujikimu kimaisha," Akothee alisema kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Mama huyo wa watoto watano amesema watoto wake ndio zawadi kubwa zaidi amewahi kupokea maishani.

Fancy Makadia ambaye ni mtoto wa tatu wa Akothee amekuwa akiendeleza masomo yake katika mojawapo ya vyuo vikuu vya kifahari jijini Paris, Ufaransa.

Prince Oyoo na Prince Ojwang pia wamekuwa wakiishi huko Ufaransa na aliyekuwa mpenzi wa Akothee na ambaye pia ni baba ya Oyoo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved