logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilikuwa na msongo wa mawazo-Flaqo afichua sababu ya kuchukua mapumziko kutoka kwa ucheshi

Flaqo alisema imekuwa safari ngumu kwake kupata nafuu na kuwa kawaida.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri29 May 2022 - 07:10

Muhtasari


  • Flaqo afichua sababu ya kuchukua mapumziko kutoka kwa ucheshi
Mchekeshaji Flaqo Raz

Mchekeshaji maarufu mtandaoni Flaqo hatimaye amefichua sababu iliyomfanya kuchukua muda wa kutayarisha maudhui na kwa nini amekuwa kimya kwa mwaka 1 uliopita.

Akizungumza katika mahojiano , Flaqo alisema kuwa alilazimika kupumzika kwa sababu ya matatizo ya afya ya akili.

Alisema kuwa alikuwa maarufu akitengeneza pesa lakini hakuwa na furaha sana, na hakuna kitu kilichokuwa kikimsisimua.

Alisema alikuwa na aina fulani ya mshuko-moyo, na angeweza tu kujipata mpweke na kumwaga machozi.

"Nakumbuka nilimaliza shoot, nakwa na hisia fulani,Bien nakili haya, nilimpogia Bien simu nikaanza kusema mambo hata hayana maana,alinipa namba ya simu ya mtaalamu, ilikuwa hisia fulani sijui niseme Bipolar au Depression, nimekuwa nikipigana na hayo kwa mwaka mmoja sasa," Alieleza Flaqo.

Flaqo alisema imekuwa safari ngumu kwake kupata nafuu na kuwa kawaida.

Amekuwa akionana na mtaalamu kwa mwaka 1 uliopita na angalau sasa mambo ni sawa. Sasa anapanga kurejea tena katika tasnia ya uundaji wa maudhui, na yuko tayari kuzindua onyesho lake mwenyewe.

Sio Flaqo pekee ambaye amejitokeza na kusema kwamba alikuwa ama amekuwa akipambana na msongo wa mawazo bali tumewaona watu mashuhuri tofauti wakisema na kukiri kwamba msongo wa mawazo ni wa kweli.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved