logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Trevor Noah ajiondoa kama mtangazaji wa kipindi cha The Daily Show

Noah amekuwa akiendesha kipindi hicho tangu kuchukua nafasi ya Jon Stewart mwaka wa 2015.

image
na Radio Jambo

Habari30 September 2022 - 10:01

Muhtasari


•Noah alisema "amefajika sana na safari yake" lakini kuna "sehemu nyingine ya maisha yangu ambayo ninataka kuendelea kuyaangazia".

•Alisema muda wa kuondoka kwake utatangazwa baadaye na kwamba ataendelea kutangaza kwa wakati huu.

Mchekeshaji mwenye asili ya Afrika kusini Trevor Noah ametangaza kujiondoa kama mtangazaji wa kipindi cha The Daily Show cha nchini Marekani.

Noah alisema "amefajika sana na safari yake" lakini kuna "sehemu nyingine ya maisha yangu ambayo ninataka kuendelea kuyaangazia".

Mchekeshaji huyo mwenye umri wa miaka 38 amekuwa akiendesha kipindi cha habari za vichekesho na mazungumzo tangu kuchukua nafasi ya Jon Stewart mnamo 2015.

Alisema muda wa kuondoka kwake utatangazwa baadaye na kwamba ataendelea kutangaza kwa wakati huu.

Noah alianza uchezaji wake katika nchi yake ya asili ya Afrika Kusini, akitoa mifululizo ya vipindi maalum na kuandaa kipindi cha usiku kabla ya kuhamia Marekani mnamo 2011.

Bado alikuwa ni mtu asiyejulikana alipochaguliwa kuchukua kipindi cha Daily Show kwenye mtandao wa Comedy Central, lakini tangu wakati huo amekuwa nyota anayetambulika kimataifa na kushinda tuzo nyingi za televisheni.

Noah alitoa tangazo hilo mwishoni mwa kipindi chake cha Alhamisi usiku, na kusababisha mishtuko kutoka kwa watazamaji wa studio. “Nakumbuka tulipoanza... watu wengi sana hawakutuamini,” alisema.

"[Kuniteua kama mtangazaji] ilikuwa dau la kichaa kufanya. Bado jambo la wazimu kufanywa, na nafikiri bado ni chaguo la wazimu Mwafrika huyu wa kubahatisha.

"Ninashukuru kwa ajili ya safari hii. Imekuwa ya kushangaza kabisa. Ni kitu ambacho sikuwahi kutarajia."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved