logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hata nikifa leo, najua inavyohisi kuwa nambari moja- Harmonize ajigamba

Harmonize amejivunia mafanikio ya albamu yake mpya 'Made For Us.'

image
na Radio Jambo

Makala08 November 2022 - 10:04

Muhtasari


•'Made For Us' imefanikiwa kupata streams zaidi ya milioni tatu kwenye mtandao wa Boom Play katika kipindi cha wiki mbili pekee.

•Mwimbaji huyo mahiri pia alijivunia albamu yake kuongoza nchini Tanzania kwenye mtandao wa Audio Mack.

Staa wa Bongo Rajab Abdul Kahali almaarufu Harmonize amejivunia mafanikio ya albamu yake mpya 'Made For Us.'

Albamu hiyo ya tatu ya bosi huyo wa Konde Music Worldwide yenye nyimbo 14 imefanikiwa kupata streams zaidi ya milioni tatu kwenye mtandao wa Boom Play katika kipindi cha wiki mbili pekee.

Konde Boy amesherehekea mafanikio hayo makubwa na kubainisha kuwa yamemfanya apate hisia za ushindi.

"Hata nikifa leo, najua inavyohisi kuwa nambari moja kwenye mchezo," alisema kwenye Instastori zake.

Alijigamba kuwa hakuhitaji utangazaji wa vyombo vya habari, matangazo mengine yoyote wala machawa kufanikisha ushindi huo.

"Ni Mungu pekee na watu wazuri waliofanikisha," alisema.

Mwimbaji huyo mahiri pia alijivunia albamu yake kuongoza nchini Tanzania kwenye mtandao wa Audio Mack.

Harmonize aliachia albamu ya 'Made For Us' mwishoni mwa mwezi Oktoba, ikiwa albamu yake ya tatu kufikia sasa.

Nyimbo katika albamu hiyo ni pamoja na;- Mwenyewe, My Way, Leave me alone, Wote, Nitaubeba, Utanikumbuka, I miss you, Die, The way you are, Miss Bantu, Best Friend, Deka, Too Much na Amelowa.

Harmonize alitoa shukran za dhati kwa mchumba wake Frida Kajala kwa kumsaidia katika utayarishaji wa albamu hiyo.

"Umeifanya akili yangu iwe na utulivu, naweza tunga mistari inayostahili. Ulifanya kazi kubwa zaidi kuboresha albamu hii. Asante na nakupenda, mke wangu na boss wangu," alimwambia kwenye Instagram.

Aidha alidokeza kwamba albamu hiyo huenda ikawa ndio yake ya mwisho kufanya nyimbo kwa lugha ya Kiswahili.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved