logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilisherehekea mwaka mpya kwa nyumba kwa miaka mitatu - Jackie Matubia huku akizawadi wazazi wake nyumba

Matubia alieleza kuwa amekuwa akitamani kuwazawadi wazazi wake nyumba kwa miaka mitatu

image
na Radio Jambo

Makala22 November 2022 - 09:55

Muhtasari


• Kwenye ukurasa wake wa YouTube, Matubia alieleza jinsi alivyokuwa na woga wakati wa kufanya maendeleo hayo.

• Matubia alieleza kuwa aliandika malengo yake mwanzoni mwa mwaka na malengo hayo yote yalitimia isipokuwa lengo la kuwanunulia wazazi wake nyumba.

Mwigizaji Jackie Matubia amezungumzia suala la kuwazawadi wazazi wake na wadogo wake nyumba.

Kwenye ukurasa wake wa YouTube, Matubia alisema jinsi alivyokuwa na woga wakati wa kufanya maendeleo hayo.

Alieleza sababu yake ya kutofichua maendeleo yake kwenye mitandao na kusema kuwa amekuwa akisubiri kutimiza lengo lake la kuwazawadi wazazi wake nyumba.

"Kwa miaka mitatu iliyopita nimekuwa nikisherehekea mwaka mpya kwa nyumba,sikuwa na pesa na mwaka jana nilikuwa mjamzito," Matubia alieleza changamoto za kuwanunulia wazazi wake nyumba.

Mke huyo wa Blessing Lung'aho alisema kuwa aliandika malengo yake mwanzoni mwa mwaka na malengo hayo yote yalitimia isipokuwa lengo la kuwanunulia wazazi wake nyumba.

Baadhi ya malengo ambayo Matubia alitumainia kufanikiwa kufanya ni kama kuvalishwa pete ya uchumba, kupata mtoto na kuwa na nyumba ya kifahari.

Mama huyo wa watoto wawili alisema kuwa aliposhindwa kuwanunulia wazazi wake nyumba kwa miaka miwili, alikuwa amehuzunika na kuvunjika moyo.

Matubia alieleza jinsi mume wake, Blessings Lung'aho alimpa nguvu kwa kumshauri na hata kwa kumtuliza alipohisi hayuko sawa.

"Nilikuwa kwenye giza, nilikuwa nimechoka. Namshukuru Mungu kwa kunipa mpenzi anayenielewa na aliyefahamu nilichokuwa ninataka sana maishani. Amekuwa akiniunga mkono nilipokuwa nikijiuliza maswali mengi," Matubia alieleza.

Aliendelea kusema kuwa hakutaka tu kuwanunulia nyumba bali pia alitaka kuwanunulia gari.

Alisema jinsi mambo mengi kama uchaguzi mkuu yalikuwa yakimzuia kununua nyumba ila hatimaye amefanikiwa kuwazawadi wazazi wake.

"Niliwasumbua wazazi wangu kitambo, unapofanikiwa, unafaa kuwalipa wazazi wako kwa yote waliyokufanyia, wape furaha," Muigizaji huyo alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved