logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Siku nitafanya collabo na Fally Ipupa, nitakuwa nimefanikiwa kimaisha - Nadia Mukami

Msanii huyo kwa sasa anashughulikia albamu yake mpya ambayo itatoka mapema mwaka kesho.

image
na Radio Jambo

Habari22 November 2022 - 07:21

Muhtasari


• Siku ambayo nitafanya collabo na Fally Ipupa, nitakuwa nimetusua kimaisha. Kwa sasa bado sana - Nadia Mukami.

Nadia azungumzia collabo ya ndoto zake na Fally Ipupa

Malkia wa muziki wa Kenya wa kizazi kipya Nadia Mukami amedhibitisha kuwa ujio wa albamu yake mpya mapema mwaka kesho maandalizi yake yameanza kwa kasi ya 5G.

Akidhibitisha hili kupitia ukurasa wake wa Instagram, Nadia Mukami alisema kuwa kwa sasa inabidi tu amewatesa kwa njaa mashabiki wake kwa muda mchache tu ila mwaka utaanza kwa fujo kubwa kwani albamu yake itasimamisha mawimbi ya soka si tu nchini Kenya bali ukanda wa Afrika Mashariki bila kusaza mataifa ya Jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo na hata Sudan ya Kusini.

Mukami alisema kuwa ndoto yake kubwa ni kuwa na mafanikio makubwa kimuziki na katu hawezi kutebwereka kama hajafanikiwa katika hilo.

Alisema kuwa ile siku atafanikiwa kufanya collabo na staa kutoka DRC Fally Ipupa basi hiyo ndio siku atajihisi kuwa angalau ameifanyia haki safari yake ya muziki na atajipiga kifua kuwa kweli mtoto wa Kenya ametusua.

“Imethibitishwa

“Ninafanyia kazi Albamu yangu! Kitu bora ninachoweza kufanya ni kuwaweka njaa mashabiki wangu kidogo tu! 😁Mapema mwaka ujao, nyote mtapata Albamu! Kutuma Upendo kwa Mashabiki wangu! kaNadians!” Nadia alisema.

“Siku ambayo nitafanya collabo na Fally Ipupa, nitakuwa nimetusua kimaisha. Kwa sasa bado sana… collabo ya ndoto zangu ni Fally,” Nadia aliongeza kwenye instastory yake.

Msanii Fally Ipupani msanii mmoja ambaye kwa sasa anatajwa kuwa mwenye ufuatiliaji mkubwa sana wa kimuziki na ndio maana kila msanii anatamani kufanya collabo naye kutoka ukanda huu.

Ikumbukwe tu kwamab msanii huyo ameshirikiana na msanii mmoja tu kutoka ukanda wa Afrika Mashariki, Diamond Platnumz, wimbo wa ‘Inama’ uliotoka miaka mitatu iliyopita na kuteka mawimbi pakubwa. Wimbo huo ulishikilia usukani kwenye chati za muziki kwa muda kutokana na ubora wake.

Kila la kheri Nadia!


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved