logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Lala salama-Mpenziwe Baha aomboleza kifo cha mmoja wa wapendwa wake

Mnamo Machi 2022, walitangaza kuwa walikuwa wanatarajia mtoto wao wa kwanza.

image
na Radio Jambo

Makala24 January 2023 - 09:04

Muhtasari


  • Georgina Njenga alifahamika sana alipoanza kuchumbiana na aliyekuwa mwigizaji wa Machachari Tyler Mbaya almaarufu Baha
Mpenzi wa Baha, Georgina Njenga arejea mitandaoni

Muunda maudhui Georgina Njenga na wapendwa wake wanaomboleza kifo cha mmoja wao.

Georgina kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram Jumatatu jioni alishiriki rambirambi zake kutokana na kifo cha nyanyake.

Georgina, ambaye hakushiriki maelezo ya kina kuhusu hali ya kifo cha bibi yake, alinukuu na kusema kuwa alikuwa nyanya yake bora.

"Pumzika kwa amani shosho, hakika bibi bora ningemtaka maishani mwangu."

Ingawa watu mashuhuri wanaweza kuwa na talanta, umaarufu, na pesa, hakuna kitu kinachoweza kuwalinda kutokana na ukweli wa kibinadamu wa huzuni na hasara.

Georgina Njenga alifahamika sana alipoanza kuchumbiana na aliyekuwa mwigizaji wa Machachari Tyler Mbaya almaarufu Baha.

Wapenzi hao wachanga wamekuwa wakitimiza malengo ya wanandoa kwa miaka miwili ambayo wamekuwa pamoja licha ya wengi kudai kuwa hawatadumu.

Mnamo Machi 2022, walitangaza kuwa walikuwa wanatarajia mtoto wao wa kwanza.

Wazazi hao wawili baadaye walimkaribisha binti yao Astra Nyambura mnamo Mei 7, 2022, na kufichua kuwa alileta furaha nyingi maishani mwao.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved