logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Naomba mke mwema lakini napata 'single mother' - Ommy Dimpoz ataja sababu ya kutooa!

Ommy Dimpoz ana miaka 35 lakini hajawahi oa wala kuwa na mtoto.

image
na Radio Jambo

Habari04 March 2023 - 10:20

Muhtasari


• Kwa kauli yake, huenda hili ndilo tatizo ambalo kwa muda limekwamisha juhudi zake za kupata mchumba.

Ommy Dimpoz ataja sababu ya kutooa

Msanii Ommy Dimpoz anahisi kwamba kuna tatizo la kiufundi kote duniani haswa ikija ni maswala ya wanaume kuomba au kutafuta wanawake wazuri wa kutulia nao katika ndoa.

Msanii huyo mwenye umri wa miaka 35 bila kiashiria chochote cha mke wala mtoto hata yule wa kusingizwa aliandika haya kupitia ukurasa wake wa Snapchat akisema kwamba wanaume wengi wamekuwa wakilipata tatizo hilo la “kiufundi” ambapo wanaomba wake wema wa kuoa lakini wanachokipata ni kina mama waliozaa na hawana wanaume.

“Sasa hivi kuna tatizo la kiufundi duniani, yaani ukiomba mke mwema unaletewa singo maza,” Ommy Dimpoz aliandika akimalizia na emoji za kucheka.

Ommy Dimpoz kwa muda amekuwa akikwepa kuzungumzia kuoa na kinachojulikana kumhusu ni mpenzi wake Maya Mia aliyefariki miezi kadhaa iliyopita, japo pia aliweka wazi kwamba walikuwa wameachana naye muda mrefu tu.

Mia alifariki katika hali ambayo haikuwekwa wazi lakini Dimpoz alikuwa mstari wa mbele kuongoza waombolezaji wengine kumuomboleza mrembo huyo.

Kwa kauli yake, huenda hili ndilo tatizo ambalo kwa muda limekwamisha juhudi zake za kupata mchumba kwani huenda amekuwa akijaribu kumtafuta mke mzuri na mwema wa kumzalia lakini anaowapata ni wale waliozaa na hawana wanaume, kwa kimombo ‘single mothers’

Lakini hayuko peke yake, wasanii wengi tu waliofanikiwa kumuziki wameshindwa kupata wake wazuri wa kuishi nao licha ya kuwa na umri mzuri wa kuingia kwenye ndoa.

Alikiba alijaribu hadi kufunga ndoa ya Kiislamu na mrembo kutoka Kenya lakini ndoa yake iliota mabua na kumalizia kusambaratika licha ya msanii huyo msiri wa mambo ya kibinafsi kuwa kimya kuhusu hilo muda wote huu.

Wasanii wengine kina Diamond, Harmonize, Rayvanny pia hawajawa na bahati kwani wamekuwa katika mahusiano mbalimbali lakini hakuna tija wamepata.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved