logo

NOW ON AIR

Listen in Live

King Kaka amlimbikizia sifa mkewe huku akisherehekea siku yake ya kuzaliwa

Katika ujumbe wake alimuahidi mkewe kuwa pamoja hadi nyakati zao za uzeeni.

image
na Radio Jambo

Makala15 March 2023 - 11:38

Muhtasari


  • Kaka amemsifia mumewe kwa urembo wake wa kipekee na kuwa mama bora kwa watoto wao.

Rappa maarufu King Kaka kupitia kwenye ukurasa wake wa facebook amemsherehekea mkewe Nana Owiti kwa ujumbe mtamu.

Licha ya kumsherehekea alimlimbikizia sifa tele, kwa kuwa mke mwema  na hata rafiki mwema.

Katika ujumbe wake alimuahidi mkewe kuwa pamoja hadi nyakati zao za uzeeni.

Wawili hao wamekuwa kwenye ndoa kwa zaidi ya miaka 5, na wamebarikiwa na watoto pamoja.

Kaka amemsifia mumewe kwa urembo wake wa kipekee na kuwa mama bora kwa watoto wao.

"Leo ni siku ya kuzaliwa ya rafiki yangu bora. Asante kwa kila kitu (unajua ninamaanisha) Mama mkubwa , Dada wa ajabu, Mpenzi mzuri wa moyo, Bibi mwenye busara, Ukuu, Mpishi wa kustaajabisha, Rafiki thabiti , Mzazi wa Kusudi, Mshangiliaji No 1, Gossip saa zingine, Urembo na Akili . Naweza kuomba nini zaidi? Heshima kufanya kitu hiki kinachoitwa maisha na wewe. Happy Birthday mke wangu kipenzi na May Happiness ikufuate na Mei matakwa yako yote yatimie. Hadi tukunje mgongo. Heri ya Siku ya Kuzaliwa Nana Owiti."

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved