logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Alikiba ashtushwa na uvumi kwamba ameshirikishwa kwenye albamu ya Davido, akanusha!

"Nadhani sijaona kama Davido amepakia kitu kama hicho." - Alikiba.

image
na Radio Jambo

Makala17 March 2023 - 07:49

Muhtasari


• "Inawezekana nifanye ngoma na Davido ndio maana watu wameeneza hilo, lakini kiuhalisia inafaa umuulize mtu" - alisema.

• Albamu mpya ya Davido inatarajiwa kutoka hivi karibuni.

Alikiba akanusha kufanya collabo na Diamond

Tangia Jumatano, kumekuwa na orodha ambayo ilikuwa inaenezwa mitandaoni ikionesha orodha ya ngoma za albamu mpya ijayo ya msanii nguli kutoka Nigeria, Davido.

Katika orodha hiyo ambayo haijulikani iliasisiwa na nani, ilikuwa ikiwaonesha wasanii mbali mbali ambao walipata nafasi ya kupewa shavu na Davido kwa maana ya Collabo, likiwemo jina la msanii kutoka Tanzania, Alikiba.

Mashabiki wa muziki haswa kutoka ukanda wa Afrika Mashariki walifurika mitandaoni wakimsifia na kumhongera Alikiba kwa kuoata nafasi adimu ya kuwa kwenye albamu inayosubiriwa mno ya Davido.

Lakini sasa Alikiba mwenyewe amejitokeza wazi akipuuzilia mbali orodha hiyo inayomuonesha kuwa yuko miongoni mwa wasanii walioshirikishwa kwenye albamu ya Davido.

Katika mahojiano na kituo kimoja cha habari nchini Tanzania, Alikiba alikanusha kufanya collabo na Davido na kusema kwamba hata kama kuna uwezekano wa kufanya collabo naye lakini hata siku moja hajawahi shirikiana naye kwenye wimbo, na hivyo kuzima uvumi huo.

“Kuna baadhi ya media ambao wanaweza wakakuza jambo bila kuwa na uhakika. Mimi sijawahi fanya wimbo na Davido. Inawezekana nifanye ngoma na Davido ndio maana watu wameeneza hilo, lakini kiuhalisia inafaa umuulize mtu. Nadhani sijaona kama Davido amepakia kitu kama hicho. Ni vitu ambavyo mimi mwenyewe vinanishangaza, mimi mwenyewe nimeshtuka kweli kweli, ni lini nilifanya wimbo na Davido?” Alikiba aliuliza.

Baada ya mfalme huyo kama anavyojiita kukanusha madai ya kufanya wimbo na Davido, inasalia kwamba Afrika Mashariki ni Diamond pekee aliyewahi kufanikiwa kuingia na Davido studioni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved