logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Lala salama kaka-Nameless ajiunga na Wakenya kumuomboleza Kunguru

Taarifa za kifo chake zimeshtua wengi na wenzake wachache wamejitokeza kuomboleza.

image
na Radio Jambo

Makala20 March 2023 - 08:52

Muhtasari


  • Mapema leo mwanamuziki maarufu Nameless aliomboleza kifo cha Kunguru
  • Akichapisha kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii, mwanamuziki huyo alionyesha kusikitishwa na kuamka na taarifa za kusikitisha za Kunguru kupita

Tasnia ya muziki nchini Kenya iko katika majonzi kufuatia kifo cha mwanamuziki mkongwe Eric Onguru anayejulikana pia kama Kunguru.

Kulingana na meneja wake wa zamani, kunguru aliaga dunia katika hospitali ya Nairobi Jumapili saa 2:00 usiku.

Meneja huyo alifichua zaidi kwamba ugonjwa wake wa muda mrefu ulisababishwa na ajali aliyopata mwaka wa 2009 iliyoathiri uti wake wa mgongo.

Taarifa za kifo chake zimeshtua wengi na wenzake wachache wamejitokeza kuomboleza.

Akichapisha kwenye mitandao ya kijamii siku ya Philip Etale pia aliomboleza akisema kwamba wengi walifurahia muziki wake siku za zamani.

Mapema leo mwanamuziki maarufu Nameless aliomboleza kifo cha Kunguru.

Akichapisha kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii, mwanamuziki huyo alionyesha kusikitishwa na kuamka na taarifa za kusikitisha za Kunguru kupita.

Alikumbuka kuwa wote wawili walikuwa wamesajiliwa katika lebo ya muziki ya Ogopa DJs mwanzoni mwa 2000 na akafichua kuwa alikuwa ameacha kumbukumbu na vibao kadhaa.

"Oh my kuamka na kupatana na habari za kusikitisha za kifo cha Kunguru,tulikuwa tumesajiliwa wote kwenye ogopa DJs lala salama kaka umetuacha na kumbukumbuku nzuri na miziki nzuri,"Aliandika Nameless.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved