logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Salasya ajumuika na Linet Toto kwa chakula, mwezi baada ya kutishia kumpachika mimba

Safari hii, wawili hao walikutanishwa na mlo wa mchana wakijiandaa kwenda Tanzania.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri28 March 2023 - 12:46

Muhtasari


• Mwezi mmoja uliopita, Salasya alijipata taabani baada ya makundi ya kina mama kumtaka kuomba radhi Toto kwa matamshi kuwa angemtunga mimba.

• Hata hivyo, Salasya alisimama kidete akisema hangeomba msamaha, lakini ni kama walisuluhisha tofuati zao kinyemela.

Wabunge Linet Toto na Peter Salasya wajumuika kwa chakula

Hatimaye mbunge wa Mumias Mashariki Peter Salasya amekutana na mbunge wa kaunti ya Bomet Linet Toto katika mgahawa kwa chakula cha mchana.

Wabunge hao walikuwa wakijipatia chakula cha mchana kabla ya kufunga safari kwenda nchi jirani ya Tanzania kushiriki michezo ya wabunge wa jumuiya ya Afrika Mashariki.

Katika picha hiyo, Salasya ambaye alikuwa na tabasamu pana usoni alikuwa akila ugali huku Toto akiwa kando yake akiwa amevalia vazi jeusi.

“Na mheshimiwa Linet Toto na Mheshimiwa Charles Ngusya, Mbunge wa Mwingi Magharibi tukielekea Tanzania timu ya kenya ya riadha ya @NAssemblyKE miongoni mwa viongozi wengine,” Salasya aliandika kwenye picha hizo kwenye ukurasa wake wa Twitter.

Hii ndio mara ya kwanza wawili hao wanaonekana hadharani tangu mwezi mmoja uliopita waligonga vichwa vya habari kuhusu uwezekano wa kuwepo kwa uhasama wa kisiasa baina yao.

Mwezi Februari, Salasya katika mkutano wa kinara wa Azimio Busia alipanda jukwaani akikashifu matamshi ya Toto kuhusu Odinga.

Salasya alitamka matamshi dhidi ya Toto ambayo makundi mengi yalisema ni kumdhalilisha mbunge huyo wa Bomet, aliposema kwamba alikuwa na nia ya kumtia mimba kama njia moja ya kumzima asiendelee kumshambulia Odinga.

“Kuna mwengine alichaguliwa kama hana pesa kama mimi, anaitwa Toto nitaenda kukaweka wiki kesho,” Salasya alisema.

Hili lilikuwa jibu kwa matamshi ya awali ya Toto katika hafla ya mbungwe wa Mogotio aliposema kwamba Odinga ni mzee aliyeanza siasa wakati hata yeye hakuwa amezaliwa, na kumtaka kutoendeleza upinzani dhidi ya serikali ya Ruto.

“Huyu mzee Raila Odinga alianza siasa zake za maandamano hata kabla sijazaliwa. Alianza siasa mwaka 1997 wakati sikuwa nimezaliwa na mpaka sasa bado anasema aliibiwa,” Linet Toto alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved