logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Milly WaJesus afichua sharti pekee litakalomfanya avae pete yake ya ndoa

Milly Wajesus afunguka kuwa atavaa pete yake ile siku @KabiWaJesus atampatia pete isiyokuwa chini ya $2300.

image
na

Yanayojiri12 May 2023 - 10:00

Muhtasari


• ”Kwa wale wanaoendelea kuniuliza mbona sina pete. Nitaanza kuvaa ile siku @KabiWaJesus atanipatia pete isiyokuwa chini ya $2300.

• Sipendi mapambo ya bei nafuu,” aliandika Milly WaJesus. 

Mwanablogu maarufu Milly WaJesus alifichua kuwa licha ya kuwa kwenye ndoa kwa zaidi ya miaka 5,hapendi kuvaa pete yake ya ndoa aliyonunuliwa na mumewe. 

Milly na Kabi walifunga ndoa mwaka wa 2017 na wakamkaribisha mtoto wao wa kwanza Taji WaJesu mnamo 2019.

Hadithi ya jinsi walivyokutana inavutia sana kwani walipatana kupitia marafiki wao wa karibu.

Kama wanandoa wengine wowote, wamekuwa na changamoto kwa miaka mingi, lakini wamezikumba na kuweza kufanikiwa.

Hata hivyo, Milly yuko kwenye hatihati ya kupata pete yake ya ndoto. Isitoshe sababu yake kuu ya kutovaa pete yoyote ile ni kwamba anaamini kuwa hapendi mapambo ya bei nafuu.

”Kwa wale wanaoendelea kuniuliza mbona sina pete. Nitaanza kuvaa ile siku @KabiWaJesus atanipatia pete isiyokuwa chini ya $2300 . Sipendi mapambo ya bei nafuu,” aliandika kwenye Instastori yake.

Hata hivyo, wanandoa hao walionekana wakitafuta pete ya Milly.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved