logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Prince Indah akutana na shabiki wake mkubwa ambaye pia ni mfanyikazi wa nyumbani

Mwanamziki Prince Indah hatimaye ameweza kupatana na shabiki yake mkubwa Adhis.

image
na

Yanayojiri18 May 2023 - 09:38

Muhtasari


• Mwanamke huyo kwa jina Adhis Marwa awali alikuwa amechapisha video akisema kuwa atanunua deta kutazama nyimbo za Prince Inda.

 

Msanii Prince Indah na Adhis

Mwanamziki wa mitindo ya Ohangla Evans Ochieng almaarufu Prince Indah hatimaye amekutana na mfanyikazi wa nyumbani ambaye awali alikuwa umemuonyesha upendo wa dhati.

Mwanamke huyo kwa jina Adhis Marwa awali alikuwa amechapisha video akisema kuwa atanunua data bundles ili kutazama nyimbo zote za msanii huyo.

Video hio ilimvutia Indah na akawaomba mashabiki wamsaidie kumpata mwanamke huyo.

Indah baadaye aliweza kupata namba yake ya simu na kumnunulia data jambo ambalo Adhis alilithamini sana.

Jumatano Indah na Adhis hatimaye waliweza kupatana kwa mara ya kwanza.

Adhis alijawa na furaha baada ya kukutana na mwanamziki huyo na hata kupata fursa ya kupiga picha naye.

Indah aliweka video katika akaunti yake ya Tik Tok iliyowaonyesha wakisakata densi pamoja.

Je, wewe ungejihisi aje kupatana na msaanii unayemuenzi?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved