logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gidi: Kwa nini mawasiliano ya FB ni magumu haswa ukiwa na hadhara mchanganyiko

Facebook sio jukwaa la mazungumzo ya mada ya kina - Gidi alisema.

image
na Radio Jambo

Habari24 May 2023 - 04:21

Muhtasari


• Mtangazaji huyo alisema hali kama hii haipo kwenye WhatsApp kwani kule hadhira ni maalum kwa sualaFulani.

Mtangazaji wa Radio Jambo katika kipindi cha asubuhi Gidi ameelezea chanzo cha ugumu wa mawasiliano ya mitandaoni haswa Facebook baina ya watu maarufu na wafuasi wao.

Gidi anahisi kwamba wakati mwingine watu wenye umaarufu mkubwa mitandaoni huwa na ugumu kufanya mawasiliano ya maana na wafuasi wao kwani mara nyingi watu hawa huwa na ufuasi wa watu kutoka kila tabaka.

Gidi alisema kwamba haswa yeye hupata wakati mgumu kuwaelewesha wafuasi wake kwani hadhira yake imechanganyikani matabaka na wakati mwingine akijaribu kuzungumzia kitu cha mzaha huwa anapoteza hadhira ya watu wasomi na wakati mwingine pia akiamua kuzungumzia kitu cha kitaaluma huwa anawapoteza wale wapenda mzaha – hivyo kuleta mkwamo mkubwa katika mawasiliano.

“Mawasiliano kwenye Facebook yanazidi kuwa changamoto, haswa ikiwa una hadhira iliyochanganyika ya umma. Wakati fulani unataka kujihusisha na mada fulani yenye kuchochea mawazo lakini kuna sehemu ya wasikilizaji wako ambayo itapotea, wengine wanaweza hata kufikiria kuwa unawanyanyasa au kuwadharau,” Gidi alihisi.

“Halafu saa zingine pia uko tu na stories za mtaa, za ma hustlers ama za spoti hivi, halafu unajikuta tena unapoteza sehemu nyingine ya watazamaji wako ambao wanaona chapisho lako ni la kina sana au halijafikia viwango vyao. Hili ni tatizo la mawasiliano pengine mahususi kwa jukwaa la Facebook.”

Mtangazaji huyo alisema hali kama hii haipo kwenye WhatsApp kwani kule hadhira ni maalum kwa sualaFulani lakini katika Facebook hadhira huwa imechanganyikana kutoka kila tabaka.

Gidi alielezea kuwa baada ya kujua hilo kwenye Facebook, ndio maana amejikita sana katika kuzungumzia masuala yote kutoka siasa, utani, spoti na mengine ya kawaida.

“Ndiyo maana huwa napenda kushikilia mada za jumla kuhusu kashfa za michezo, habari laini, kejeli au vicheshi tu vya mtandaoni. Facebook sio jukwaa la mazungumzo ya mada ya kina,” Gidi alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved