06 October 2015 1 Min Read
KIRINYAGA: Mwanamme Alazwa Baada Ya Kuchomwa Na Mkewe
by Michael Mutai Habari
Mafuta ya taa. | picha: indianexpress.com
Mwanamme mmoja amelazwa katika hospitali moja huko Kirinyaga baada ya kuchomwa na mkewe walipogombana kufuatia mzozo wa kinyumbani.
Inadaiwa kuwa mkewe alisubiri hadi mwathiriwa alipolala kisha akamwagia mafuta ya taa na kuwasha moto kabla ya kutoroka.
Polisi wameanzisha uchunguzi kwa kisa hicho na wanamsaka mwanamke huyo.