Mwendeshaji mmoja wa pikipiki mwenye umri wa makamo huko Mwatate kaunti ya Taita Taveta ameaga dunia papo hapo usiku wa kuamkia leo baaada ya kugonga trella kwa nyuma katika barabara ya Mwatate/Taveta.

Walioshuhudia wanasema mwendazake alikuwa anajaribu kuipita trella hiyo kabla ya kupunguza mwendo ili kukwepa kugongana ana kwa ana na gari jingine.

Mwili wake umepelekwa kuhifadhiwa katika hifadhi ya Moi mjini Voi.

Solomon Muingi Junior

View Comments