1894151

Polisi waliniweka pilipili katika sehemu zangu za siri kwa kushukiwa kumuuwa mwanabiashara Mary Wambui, mahakama ilisikiza jana.

Judy Wangui alisema kuwa Polisi hao walitaka kumlazimisha kubadilisha kauli yake ya awali,  kupitia kwa wakili wa Wangui Cliff Ombeta, aliambia hakimu mwandamizi mkuu wa mahakama ya Kiambu Stella Atambo kuwa Judy aliteswa katika kituo cha polisi cha Juja.

Alisema kuwa polisi wawili wanawake walimdhalilisha Ijumaa usiku.

Mahakama ilisikia kuwa Judy alikuwa na alama katika mapaja yake na katika mwili wake na kusema kuwa ripoti ya kudhalilishwa iweze kuletwa tarehe itakayo tajwa.

Pia mahakama hiyo iliweza kuwapa wachunguzi siku tisa iliweze kushikilia washukiwa hao walio hisika na mauaji ya mwanabiashara huyo mpaka tarehe 27 Februari kesi itakavyo tajwa.

Mashtaka iliweza kuambia hakimu huyo kuwa uchunguzi ni mgumu kwa hivo wanataka wakati mwafaka. hii ni kabla ya wakili wa washukiwa kupinga, na kusema kuwa hakuna jambo lolote polisi wanafanya.

Washukiwa ni Wangui mpenzi wa kori, Josepj Kori mume wa mwendazake Mary na Michael Mathenge ambaye alisema kuwa aliweza kuwasaidia kuupeleka mwili wa Mary katika mto Juja.

Mahakama iliweza kuuliza bidhaa ambavyo vili chukuliwa nyumbani mwa kori ziweze kuletwa mahakamani.

Jana mume wa Mary Joseph Kori, 41, ambaye ni mshukiwa mkuu aliweza kulia mbele ya mahakama bila kuzuia machozi yake, aliweza kuzuia machozi yake.

Kori alikuwa anafanya mzuri mpaka wakati ambao wakili wake aliweza kusema mbele ya mahakama, akiwakilisha kesi yake alitoa kitambaa cheupe na kupanguza machozi yake.

Wambui aliweza kutoweka Januari, 26, na mwili wake kupatikana siku baada ya kutoweka kwake katika hoteli ya Courtesy Beach eneo la juja.

Katika filamu iliyosambaa kwa mitandao siku baada ya mauaji hayo ya kikatili Mary, 39, aliweza kuwapa watu motisha kuwa changamoto si za kila siku ama kila wakati.

View Comments