Mwanamume mmoja amemuua mkewe katika kijiji cha mahiakalo kaunti ya kakamega na kisha kutorokea katika msitu wa Kakamega akitishia kijutia kitanzi

Juhudi za jamaa yake kumpata hazijafua dafu.

Kwingineko

Serikali imewatahadharisha wananchi dhidi ya kupotoshwa kuhusu mpangilio wa serikali wa kuwasajili wakenya kwa nambari maalum

Justus Mukoshi kutoka idara ya utawala kaunti ya kakamega amewasuta baadhi ya watu wanaowapotosha wananchi kuwa serikali ina nia tofauti ya kuwasajili katika nambari hiyo yakiwemo mambo ya kura ya maoni

Kwingineko

Makundi ya kijamii na idara za elimu na mahakama katika kaunti ya Taita Taveta zimetakiwa kushirikiana ili kukomesha ongezeko la visa vya dhulma za kijinsia dhidi ya watoto katika eneo hilo.

Macrina Mwamburi kutoka sauti ya wanawake anasema visa hivyo bado vinaendelea kuripotiwa kwa wingi hususan maeneo ya mashinani huku washukiwa wakikosa kuchukuliwa hatua za kisheria.

Anasema kuna haja ya jamii kupewa hamasa kuhusu athari za uovu huo.

View Comments